Watu 38 wauawa katika milipuko miwili mjini Jos Nigeria
Takriban watu 46 wameaga dunia
na wengine wengi kujeruhiwa baada ya milipuko miwili mikubwa kutokea
nchini Nigeria katika mji wa Jos.Milipuko hiyo imetokea katika soko
lenye shughuli nyingi .
Mwandishi wa BBC aliyeko huko anasema kuwa
amehesabu miili 40 ikipelekwakatika chumba cha kuhifadhia maiti katika
hospitali moja iliyoko JOS.
Mwandishi wa BBC Ishaq Khalid aliye
mjini humo anasema kuwa kuna hofu ya watu wengi kujeruhiwa hasa kwa kuwa
soko hilo lilikuwa na idadi kubwa ya watu.
Aidha anaarifu kuwa taharuki ietanda katika eneo
hilo baada ya vijana waliopandwa na hasira kufunga mabarabara ya
kuingia na kutoka mjini humo na kuzua hofu ya makabiliano.
Mji wa Jos itakumbukwa iliwahi kushuhudia
mapigano mabaya zaidi baina ya makundi ya vijana Waislamu na wale
Wakristu iliyosababisha maafa mengi.
Mabomu hayo yanasemekana kuwa yalikuwa yametegwa
moja katika lori na lingine katika gari la uchukuzi wa abiria na
yakalipuka kwa mpigo moja katika soko la lingine karibu na hospitali.
Hakuna aliyekiri kutekeleza mashambulizi hayo
ijapokuwa jimbo hilo limewahi kushambuliwa na kundi la Boko Haram zaidi
ya miaka miwili iliyopita.

Watu 38 wauawa katika milipuko miwili mjini Jos Nigeria
Watu 38 wauawa katika milipuko miwili mjini Jos Nigeria
Jimbo la Platue liko mpakani kati ya waislamu wanaoishi Kaskazini mwa Nigeria na Wakrstu ambao wanaishi Kusini .
Jimbo hili limewahi kushudia mapigano baina ya
wakulima wakristu wa tabaka la Berom na waislamu wafugaji wa kuhamhama
wa tabaka la Fulani.
Mnamo mwezi Machi mwaka uliopita kituo cha basi
kilishambuliwa kwa bomu na awali mwaka wa 2012, Boko Haram walifanya
shambulio baya zaidi lililowaua zaidi ya watu 150 katika msururu wa
milipuko.
Kundi hilo bado linawazuilia wasichana zaidi ya
200 wa shule, lililowateka kutoka kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa
Nigeria mwezi mmoja uliopita.
Nchi kadhaa zikiwemo Uingereza, Ufaransa na Marekani wameahidi kutuma wanajeshi kusaidia kuwakomboa wasichana hao.
Nao viongozi wa Afrika wanaokutana mjini Paris
wametangaza 'vita' dhidi ya Boko Haram na kuahidi kushirikiana
ki-intelijensia na kijeshi, kupambana na Boko Haram.