BBC imeitaka serikali ya Urusi kuchunguza tukio hilo dhidi ya wandishi wake

BBC imewasilisha malalamiko kwa serikali ya Urusi baada ya wandishi wake wa habari kushambuliwa Kusini mwa nchi hiyo.

Wandishi hao walikuwa nchini Urusi kuchunguza madai ya baadhi ya maafisa wa usalama wa Urusi kuuawa karibu na mpaka na Ukraine.

Baada ya kuwaarifu maafisa wa huduma ya dharura , waandishi hao walipelekwa katika kituo cha polisi na kuhojiwa kwa saa nne.

Picha walizokuwa wamenasa kwenye kamera zilifutwa wakati wakiwa kwenye kituo cha polisi.

BBC inasema kuwa imechukizwa na kitendo hicho na kutoa wito kwa maafisa wa utawala nchini humo kuchunguza taarifa hizo pamoja na kuwataka kulaani kitendo hicho.
Wascochi wanapiga kura kuamua ikiwa wataendelea kuwa sehemu ya Uingereza au watajitawala

Wapiga kura wamekuwa wakielekea kwa vituo vya kupigia kura katika maeneo mbali mbali nchini Scotland, ambapo watu wanaamua leo ikiwa wataendela kuwa sehemu ya uingereza au wawe taifa huru kwa mara ya kwanza kabisa tangu zaidi ya miaka 300 iliyopita.

Mwandisi wa bbbc anasema kuwa siku ya leo inatarajiwa kuwa ya shughuli nyingi katika historia ya kupiga kura eneo la Scotland ikiwa asilimai 97 ya watu wamejisajili kupiga kura.

Kumekuwa na kampeni kali katika saa 24 zilizopita huku ikidhihirika matokeo yanaweza kwenda upande wowote.

Kiongozi wa chama cha Scotish National Party, Alex Salmond, ametaja kampeni ya kuitisha Uhuru wa Scotland kutoka kwa Uingereza kama tukio muhimu zaidi la kidemokrasia kuwahi kutendeka nchini humo.

Kadhalika amesema tayari limebadilisha mfumo wa maisha eneo la Scotland.

Idadi kubwa ya wapiga kura wamesajiliwa na kwa mara ya kwanza vijana wenye umri wa miaka 16 na 17 wataruhusiwa kupiga kura.



Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wanatarajiwa kumaliza bonanza liloanza siku ya jumatano chuoni hapo 
Akizungumza na BLog hii kwa nyakati tofauti mwalimu wa michezo chuoni hapo amesema kuwa mashindano yaliyoandaliwa na kamati ya michezo yana malizika leo.
Baadhi ya michezo iliyokuwamo ni mpira wa miguu,netball,kucheza karata,kula,kuzunguka viti,kucheza draft na mingine mingi.Alisema lengo ni kutafuta timu bora ya chuo pamoja na kuwafanya wanafunzi kuwa vizuri kiafya na kiakili kwani michezo hujenga mwili kwa kufanya mazoezi.
Pia waalimu wa chuo hicho walihusishwa kwenye mashindano hayo kwa kupewa dhamana ya kuwa marefa kwenye mpira wa miguu pamoja na netball.
Wanafunzi wa chuo hicho walionyesha ushirikiano mzuri kwa kuwashabikia wenzao walipokuwa wakicheza.
Zawadi za washindi wote kwa ujumla zitatolewa leo chuoni hapo baada ya kumalzika kwa michezo yote...



MBUNGE wa Urambo Magharibi, Prof. Juma Kapuya (CCM), ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi wa zamani, jana alijikuta katika wakati mgumu wa kuumbuliwa na mbunge mwenzake wa Temeke, Abbas Mtemvu (CCM), wakati wawili hao wakibishania uuzwaji tata wa Kampuni ya Usafiri Dar es Salaam (UDA).Hatua hiyo ilijitokeza wakati Mtemvu akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa mwaka wa fedha 2014/2015, na kuungana na wabunge wenzake kadhaa waliotangulia kuchangia, akidai UDA imeuzwa kifisadi bila wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam kushirikishwa.
 Wakati Mtemvu akiendelea kujenga hoja yake, Prof. Kapuya aliomba kumpa taarifa, akimweleza kuwa mbunge kujishughulisha na uwekezaji si dhambi na kwamba UDA imeuzwa kihalali wala hakuna ufisadi kama inavyodaiwa, isipokuwa mbunge huyo anatumika kuwashawishi wabunge kupinga suala hilo. Baada ya Prof. Kapuya kuketi,



Mtawa wa Italia anyakua ushindi
Mtawa mmoja kutoka Italia ambaye alipata umaarufu katika mtandao wa kijamii ameshinda shindano la kuimba nchini humo.
Mtawa huyo, Sister Christina Scuccia alitokea kwa mara ya kwanza katika televisheni kushiriki shindano la The Voice.
Scuccia aliyeonekana amevalia mavazi yake ya utawa na msalaba shingoni, alijawa na furaha na kumshukuru Mungu kwa kumfikisha katika ushindi huo.
Mtindo wake wa wimbo wa Alicia Keys, kwa jina 'No One', umetizamwa zaidi ya mara milioni 50 katika mtandao wa You Tube tangu auimbe.
Mtawa huyo mwenye umri wa miaka 25 amesema kuwa aliamua kushiriki mashindano hayo kufuata ushauri wa Papa mtakatifu Francis, kuwa kanisa liwakaribie zaidi watu wa kawaida.

wanawake wa Misri
Kwa mara ya kwanza Misri imepitisha sheria inayotaja unyanyasaji wa wanawake kuwa uhalifu.
Chini ya sheria hiyo wanaume watafungwa miaka 5 gerezani kwa kuwanyanyasa wanawake hadharani au faraghani.
Sheria hiyo imepitishwa kama hatua ya mwisho kuchukuliwa na rais anayeondoka wa Misri Adly Mansour.
'Unyanyasaji umezidi'
Watetesi wa haki za wanawake nchini Misri wamesema kuwa unyanyasaji wa wanawake umefikia viwango vya kuhuzunisha. Utafiti uliofanywa umeonesha kuwa karibu wanawake wote wa Misri wamewahi kupitia unyanyasaji wa aina fulani iwe ya matusi au hata ubakaji.
Utafiti huo umeonesha kuwa hata mavazi ya kufunika mwili wote yanayopendekezwa na sheria za kiislamu nchini humo, hazijawazuia wanaume hao kuwanyanyasa wanawake.
Na sasa inahofiwa kuwa mapinduzi waliofanya mwaka wa 2011 hayakuleta mabadiliko yoyote.
Wanawake wengi wamelalamika kuwa walinyanyaswa wakiwa katika maandamano katika midani ya Tahrir.
'Tatizo liko kwa itikadi mbovu'
Watetesi hao wa haki wanasema kuwa polisi mara nyingi wanawalaumu waathiriwa kuliko wale wanaofanya uhalifu huo.
Sasa sheria hii inachukuliwa kama hatua kubwa sana kusaidia tatizo hilo, ila hofu ni kwa utekelezaji wake. Wadadisi wanasema kuwa itakuwa vigumu zaidi kubadilisha itikadi za watu juu ya unyanuasaji wa wanawake nchini humo .
mkutano wa G7
Viongozi wa mataifa tajiri ya magharibi wanaokutana mjini Brussels wamesema kuwa wako tayari kuweka vikwazo zaidi kwa Urusi iwapo itaendelea kuvuruga amani mashariki mwa Ukrain.
Taarifa ya pamoja ya mataifa ya G7 imesema kuwa Mambo yanayofanywa na Urusi nchini Ukrain hayawezi kubalika kamwe na lazima yakomeshwe.
Huu ndio mkutano wa kwanza wa viongozi hao tangu waifukuze Urusi kama mwanachama.
Urusi ilibumburushwa kutoka G7 kwa kosa lake kubwa zaidi, kuinyakua Crimea kutoka Ukrain.
Viongozi wa mataifa hayo ya G7 wanakutana sasa kwa mara ya kwanza tangu wakati huo.
Ukrain vita vimechacha
Lakini huku wakikutana mapigano yamechacha kati ya serikali ya Ukrain na majeshi yanayo unga mkono Urusi mashariki mwa Ukrain.
Urusi imeendelea kukana kuhusika na mapigano hayo. Miongoni mwa mikutano iliyopangwa Alhamisi hii, waziri mkuu wa Uingereza Davin Cameron atakutana na rais Obama mjini Brussels, ambapo kwa upana zaidi watazungumzia Urusi. Kisha baada ya mkutano huo, David Cameron ataelekea Paris Ufaransa kwa mkutano wa faragha na rais wa Urusi Vladmir Putin.
Katika wiki hii mataifa ya Uropa yamekuwa yakiadhimisha siku ya kuikomboa bara Uropa kutoka utawala wa ki Nazzi katika vita vya pili vya dunia miaka 70 iliyopita.
Huku hayo yakitokea, juhudi za kidiplomasia zimeshika kasi miongoni mwa mataifa ya magharibi kumaliza uhasama kati yao na Urusi.
G7 wamepongeza uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Ukrain na wameirai Urusi kumpokea na kushirikiana na rais mpya wa Ukrain Petro Poroshenko. Pia wameonya kuwa hawatasita kuiwekea Urusi vikwazo zaidi iwapo itakataa kusaidia kurejesha uthabiti Ukrain.
Itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka 17 ambapo G7 inakutana bila Urusi.

NAIBU Meya wa Jiji la Arusha, Prosper Msofe na Diwani wa Kata ya Levelos, Ephata Nanyaro, wote kutoka CHADEMA, wamefikishwa mahakamani kwa kosa la kumshambulia mgambo wa jiji, William Mollel.
Mwanasheria wa Serikali, Mary Lucas, aliwasomea shitaka hilo la jinai namba 413/2014  jana mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Arumeru, Patricia Kisinda.
Alisema kuwa Aprili 16 mwaka huu, wakiwa maeneo ya Levelos, madiwani hao wanadaiwa kumpiga, Mollel kifuani na sehemu mbalimbali za mwili, hivyo kumsababishia maumivu mwilini.
Lucas alisema kuwa upelelezi wa shauri hilo haujakamilika, hivyo akaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa kwa shauri hilo, huku akiweka wazi kuwa upande wa serikali hauna pingamizi ya dhamana kwa washitakiwa hao.
Madiwani hao walikana shitaka hilo na wako nje kwa dhamana hadi upelelezi utakapokamilika ambapo shauri hilo litarudi mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa Julai 8, mwaka huu.
Katika hatua nyingine, wananchi kadhaa walionekana wakiwa na barua kwa ajili ya kuwadhamini madiwani hao ambao juzi walitangaza kuwa hawako tayari kudhaminiwa ili waende mahabusu kwenye gereza la Kisongo.
Wanafunzi walitawanywa kwa kutumia gesi ya kutoa machozi
Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Kenya wamezua vurugu wakipinga mpango wa serikali kutaka kuongeza karo katika vyuo vikuu vyote vya umma.
Polisi walipambana na wanafunzi hao kwa kutumia gesi ya kutoa machozi kutawanya wanafunzi hao ambao walizua vurugu mjini na kuwapora abiria huku wakiharibu magari ya umma na yale ya abiria katika barabara kuu ya Uhuru katikakati ya jiji la Nairobi.
Pia waliripotiwa kuvunja maduka na kuharibu mali ya watu.
Wachuuzi walilazimika kuondoka mjini huku polisi wakipambana na wanafunzi hao ambao waliungana kutoka vyuo vikuu mbali mbali kote nchini Kenya.
Awali maandamano yao yalikuwa salama ingawa baadaye wanafunzi hao walioanza kuandamana tangu saa nne asubuhi walianza kuzua rabsha na kulazimisha polisi kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya.
Wanafunzi hao wanaandamana kupinga mapendekezo ya serikali kuongeza karo ya vyo vikuu , ingawa waziri wa elimu ya juu Profesa Jacob Kaimenyi amesema kuwa serikali bado haijatoa tamko rasmi ikiwa wanafunzi wa vyuo vikuu watalazimika kuongeza karo.
Alisema kuwa ripoti kuwa karo itaongezwa sio sawa na ni za kupotosha akisisitiza kuwa ikiwa jambo kama hilo litafanyika litahitajika kutangazwa na baraza la vyuo vikuu nchini humo baada ya makubaliano kufikiwa.
Wanafunzi hao wanapinga mpango wa serikali wakisema kuwa kuambatana na mfumuko wa bei, karo yao haipaswi kuongezwa na kwamba serikali inapaswa kushauriana nao kabla ya kufikia hatua zozote za kuongeza karo.
Wanafunzi watano wameripotiwa kujeruhiwa katika vurugu hizo



Mashada yakiwa tayari juu ya kaburi la marehemu Adam Philip Kuambiana, muda mfupi baada ya shughuli za maziko kukamilika.

Jacob Steven 'JB', akiweka shada kwenye kaburi. 
Msanii wa fialmu Bongo, Mariam akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Kuambiana.
Mwili wa marehemu Kuambiana ukiwasili makuburini tayari kwa shughuli za kuusitiri.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Kuambiana likishushwa kaburini.
Jeneza likishushwa kaburini.
Msanii wa filamu, Richie Richie akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Kuambiana.
Baadhi ya mafundi wakichanganya zege kujengea kaburi.
Mafundi hao wakikamilisha shughuli za kujengea kaburi hilo.
Mchungaji akiweka msalaba kwenye kaburi.

 
Watu 38 wauawa katika milipuko miwili mjini Jos Nigeria
Takriban watu 46 wameaga dunia na wengine wengi kujeruhiwa baada ya milipuko miwili mikubwa kutokea nchini Nigeria katika mji wa Jos.Milipuko hiyo imetokea katika soko lenye shughuli nyingi .
Mwandishi wa BBC aliyeko huko anasema kuwa amehesabu miili 40 ikipelekwakatika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali moja iliyoko JOS.
Mwandishi wa BBC Ishaq Khalid aliye mjini humo anasema kuwa kuna hofu ya watu wengi kujeruhiwa hasa kwa kuwa soko hilo lilikuwa na idadi kubwa ya watu.
Aidha anaarifu kuwa taharuki ietanda katika eneo hilo baada ya vijana waliopandwa na hasira kufunga mabarabara ya kuingia na kutoka mjini humo na kuzua hofu ya makabiliano.
Mji wa Jos itakumbukwa iliwahi kushuhudia mapigano mabaya zaidi baina ya makundi ya vijana Waislamu na wale Wakristu iliyosababisha maafa mengi.
Mabomu hayo yanasemekana kuwa yalikuwa yametegwa moja katika lori na lingine katika gari la uchukuzi wa abiria na yakalipuka kwa mpigo moja katika soko la lingine karibu na hospitali.
Hakuna aliyekiri kutekeleza mashambulizi hayo ijapokuwa jimbo hilo limewahi kushambuliwa na kundi la Boko Haram zaidi ya miaka miwili iliyopita.

Watu 38 wauawa katika milipuko miwili mjini Jos Nigeria

Watu 38 wauawa katika milipuko miwili mjini Jos Nigeria
Jimbo la Platue liko mpakani kati ya waislamu wanaoishi Kaskazini mwa Nigeria na Wakrstu ambao wanaishi Kusini .
Jimbo hili limewahi kushudia mapigano baina ya wakulima wakristu wa tabaka la Berom na waislamu wafugaji wa kuhamhama wa tabaka la Fulani.
Mnamo mwezi Machi mwaka uliopita kituo cha basi kilishambuliwa kwa bomu na awali mwaka wa 2012, Boko Haram walifanya shambulio baya zaidi lililowaua zaidi ya watu 150 katika msururu wa milipuko.
Kundi hilo bado linawazuilia wasichana zaidi ya 200 wa shule, lililowateka kutoka kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa Nigeria mwezi mmoja uliopita.
Nchi kadhaa zikiwemo Uingereza, Ufaransa na Marekani wameahidi kutuma wanajeshi kusaidia kuwakomboa wasichana hao.
Nao viongozi wa Afrika wanaokutana mjini Paris wametangaza 'vita' dhidi ya Boko Haram na kuahidi kushirikiana ki-intelijensia na kijeshi, kupambana na Boko Haram.


“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho (leo), kuwaombea ndugu zetu.
Kholani alisema pia Mbunge wa Singida Magharibi, Mohamed Missanga ametoa Sh600,000 na wakazi wa Tarafa ya Ihanja waishio jijini Dar es Salaam pia wamechanga Sh600,000.

 Uongozi wa Kampuni ya Mabasi ya Sumry ya Sumbawanga, Rukwa umetoa ubani wa Sh5.5 milioni kwa familia za ndugu na jamaa waliofariki dunia kutokana na ajali ya moja ya mabasi yake iliyotokea Aprili 28 katika Kijiji cha Utaho, Wilaya ya Ikungi, Singida.
Katika ajali hiyo, watu 19 wakiwamo polisi wanne, walifariki papohapo baada ya kugongwa na basi hilo lililokuwa likitoka Kigoma kwenda Dar es Salaam.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza iliyolihusisha lori na mwendesha baiskeli ambaye alipoteza maisha katika eneo hilo baada ya kugongwa na lori hilo. Wakazi hao waliogongwa walikuwa wamekusanyika kushuhudia ajali hiyo.
Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Hipoliti Daniel Kholani alisema rambirambi hiyo ilikabidhiwa kwa Serikali ya Kijiji na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone ambaye naye alichangia Sh100,000.
Kholani alisema pia Mbunge wa Singida Magharibi, Mohamed Missanga ametoa Sh600,000 na wakazi wa Tarafa ya Ihanja waishio jijini Dar es Salaam pia wamechanga Sh600,000.
“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho (leo), kuwaombea ndugu zetu.”
Kholani alisema wakazi wa kijiji hicho, Mussa Mohammed, Suku Abdallah na Ayubu Ramadhani bado wamelazwa hospitalini wakiendelea kutibiwa majeraha waliyoyapata kwenye ajali ya basi hilo ambalo bado lipo Kituo cha Polisi Ikungi.
 

Aeleza umuhimu wa wananchi kuvumiliana katika mjadala hata kama watahitilafiana.

  Rais mstaafu, Benjamin Mkapa amewataka Watanzania kuwa waangalifu ili mchakato wa Katiba Mpya usiwe sababu ya kupigana au kufarakana ili kupata Katiba itakayoendelea kudumisha amani, upendo, utulivu na ushirikiano.


Mkapa alitoa wito huo juzi, alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi nyumba 30 za watumishi wa vituo vya huduma ya afya mkoani hapa zilizojengwa na Taasisi ya Mkapa HIV/AIDS Foundation kwa zaidi ya Sh1.9 bilioni.


“Vyovyote mchakato wa Katiba utakavyoishia, tuhakikishe tunabaki na amani na utulivu wetu kwa ajili ya ustawi wa nchi yetu, tuhitilafiane bila kupigana,” alisema.


Alisema Watanzania wanapaswa kwa pamoja wasiiharibu nchi yao na kuhakikisha kizazi cha sasa na kijacho, vinaendelea kuwaenzi waasisi wa Taifa kwa uadilifu mkubwa.


Akabidhi nyumba


Akikabidhi nyumba hizo, Mkapa alisema ana imani wananchi wanaohudumiwa na zahanati 15 zilizojengewa nyumba hizo wataendelea kufaidika na huduma bora kwa kuwa watumishi wameboreshewa mazingira ya kazi.


“Kama mnavyoona nyumba hizi ni za kisasa, zina maeneo muhimu yote yanayokidhi mahitaji ya binadamu, zipo imara na zimekidhi viwango vya ujenzi vinavyostahili,” alisema.


Aliitaka halmashauri zinazohusika kuhakikisha nyumba hizo zinatumika kama ilivyokusudiwa, kutunzwa vizuri na kutengewa bajeti ya kutosha kwa ajili ya ukarabati pale utakapohitajika ili ziweze kudumu kwa muda mrefu.


Vijiji vilivyonufaika vipo katika wilaya za Singida Vijijini, Iramba na Manyoni.



MAKALA YA AFYA:Wanaharakati wamepinga vikali kuwaua Nguruwe wakisena ni kinyume na haki za wanyama 


 


Asema atachagua chama chochote na ataamua baadaye awanie upande gani

  Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed amesema anapanga kujitosa kwenye kinyang’anyiro cha urais katika Uchaguzi Mkuu mwakani.


Akizungumza katika mahojiano maalumu hivi karibuni mjini Dodoma, Hamad Rashid alisema: “Kama Mwenyezi Mungu akinijalia uhai na uzima mwakani, ninatarajia kuingia kwenye kinyang’anyiro cha urais ama wa Muungano au wa Zanzibar.


“Ila sijaamua kama ni Bara au Zanzibar; kama ni chama cha CUF au kingine, hayo yote yatakuja baadaye,” alisema Hamad Rashid.


Mohamed ambaye ana mgogoro mahakamani na chama chake cha CUF, ametoa kauli hiyo wakati tayari viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), CUF kikiwamo wanajipanga kusimamisha mgombea mmoja wa urais katika uchaguzi ujao.


Mbali na CUF, vyama vingine vinavyounda Ukawa ni NCCR-Mageuzi na Chadema ambavyo pia vinakusudia kusimamisha mgombea mmoja kwa nafasi za ubunge na udiwani, lengo likiwa kukabiliana na nguvu ya chama tawala, CCM.


Hamad Rashid aliyekuwa Mjumbe wa Baraza Kuu CUF, alifutwa uanachama Januari 4, 2012 na Baraza la Uongozi la chama hicho kwa madai ya kukihujumu kwa mujibu wa kifungu 63 (1) (j) na 64 (1-5) cha Katiba ya CUF. Wengine waliotimuliwa pamoja na Hamad ni Doyo Hassan Doyo, Shoka Hamis Juma na Juma Said Sanani.


Sakata la Hamad kuvuliwa uanachama lilianza baada ya kutangaza kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa chama hicho katika uchaguzi wa mwaka huu, nafasi inayoshikiliwa na Seif Shariff Hamad ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais, Zanzibar.


Hata hivyo, Januari 10, 2012 Hamad Rashid na wenzake waliiomba Mahakama iwatie hatiani wadhamini wa CUF, kwa kukiuka amri ya Mahakama kutokana na uamuzi wa Baraza la Taifa la Uongozi la chama hicho kuwafukuza uanachama wakiwa tayari wameweka zuio.


Baadaye Septemba mwaka jana, Hamad alikaririwa na gazeti moja akisema suluhu yake na CUF haiwezi kupatikana kwa kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo hakubaliani nayo ndani ya chama hicho.





Maafisa nchini Nigeria wanasema kuwa watu 19 wameuawa baada ya mlipuko kutokea katika kituo cha basi katika mji mkuu wa taifa hilo Abuja.

Kwa mujibu wa mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, watu 60 walijeruhiwa vibaya lakini sitaka kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Amesema kuwa magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.

Mlipuko huo umetokea katika eneo la Nyanya, karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu sabini waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.

Ripoti za awali zimesema kuwa watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Waliojeruhiwa walikimbizwa hosipitalini


Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari. Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa. Hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja

Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Lakini shambulizi la bomu la tarehe 14 Aprili lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao.



Hot news is that staa ray the great leo kupitia mitandao ya jamii alizungumza kuwa anampenda sana chuchu hans, na hakuna atakayeweza kuwatenganisha, na kwa kuliaprove hilo ndipo alipoamua kuweka picha hii yapo juu ikiwa ni ishara ya mahaba na upendo kwao.


Lupita alishinda tuzo ya Oscar kwa kipawa chake cha kuigiza katika filamu 12 Years a Slave

Jarida la People limemtangaza Mkenya Lupita Nyong’o kama mwanamuke mrembo zaidi duniani mwaka 2014.

Lupita ambaye alishinda tuzo ya Oscar kwa uigizaji wake katika filamu '12 years a slave,' yuko kwenye ukurasa wa juu zaidi wa makala ya wiki hii ya jarida hilo.


Katika orodha yake ya wanawake 50 warembo duniani,Lupita amewapiku waigizaji maarufu akiwemo Kerry Washington, ambaye pia alishiriki katika filamu hiyo na mwanamuziki Pink ambao walikuwa katika nafasi ya 10 na 5 mtawalia.



Jarida la People limemtaja Lupita kuwa mwanamke mrembo

Stacy Kiebler ambaye alisifika sana kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na muigizaji nyota George Clooney, alishikilia nafasi ya nane.

Hatua ya Jarida la People ambalo huchapishwa kila wiki nchini Marekani na kusomwa na karibu watu milioni 40, kumkubali Lupita kama mwanamke mrembo duniani, ni kama tuzo kivyake kwa muigizaji huyo ambaye amegonga vichwa vya habari nchini Marekani tangu kushinda

Mtandao wa People.com, unasema kuwa muigizaji huyo alifurahia sana kutajwa na jarida hilo kama mwanamke mrembo hasa kwa sababu wasichana kama yeye watapata kuwa na matumaini ya kufanikiwa maishani kama yeye.

"Nimefurahi sana na hii ni fursa kuwafanya wasichana wengine wajihisi kuwa wana uwezo wa kufiia chochote maishani mwao.
Taarifa zinazohusiana


Stakabdhi za CIA Kufichuliwa kwa umma
Bunge kufichua siri za CIA
Kamati ya bunge la Marekani kuhusu ujasusi imeidhinisha kuwekwa wazi kwa sehemu mojawepo ya ripoti iliyoiita ya "ukatili" ilioelezea jinsi maafisa wa shiriki la upelelezi la Marekani CIA linavyowahoji wanatuhumiwa wa ugaidi.
Lakini wanakamati wanasema kuwa itachukua muda kabla ya uchunguzi huo kuwekwa wazi kwa umma.
Sehemu ya ripoti iliyofichuliwa inasema kuwa idara ya CIA kila mara ilipotosha serikali kuhusiana na mtindo wake wa kuhoji washukiwa wa ugaidi wakati wa utawala wa Rais George W Bush.
CIA inapinga baadhi ya matokeo ya taarifa hiyo huku ikikiri kutenda matendo ambayo hayakuafikiana na sera za Marekani.
Mwenyekiti wa kamati hiyo ya baraza la Senate Dianne Feinstein anasema matokeo ya kura iliyopigwa kuhusu ripoti hiyo inaonesha wabunge 11-3 waliipigia mswada huo kura huku akisema ni uchunguzi wa matokeo yanayotamausha.
 
Stakabdhi za CIA Kufichuliwa kwa umma
"ripoti hiyo inaonyesha dhuluma inayoenda kinyume na hadhi ya taifa letu,''alisema Dianne
Hii inatia doa historia ya taifa letu na ambayo hairuhusiwi kamwe kufanyika. ''Hivi sivyo wamarekani wanavyofaa kufanya." Mwanasiasa huyo wa chama cha Democrat kutoka Carlifonia amesema.
Taarifa ya wanahabari inasema kuwa japo baadhi ya wanakamati wa chama cha Republican walikashifu ripoti hiyo kwa pamoja na wa Democrats, kulionyesha waziwazi mgawanyiko uliopo ndani ya wajumbe hao.
Matokeo ya uchunguzi huo uliyomo katika kijitabu cha ukurasa 500, yatatumwa kwa Rais Barack Obama ili kuchunguzwa, kutiwa saini, kisha kutolewa kwa umma.
Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz