Kuna tofauti kubwa kati ya mabinti wa UDSM na wale wa UDOM. Mbali na kwamba wote ni wazuri na wamemeenda vidato lakini zipo tofauti kubwa baina yao zinazowatofautisha. Kwa ujumla tofauti zao ni hivi zifuatazo;

Muonekano (image)
Binti wa UDSM mara nyingi atapenda avae vitu mpaka aonekane kama mwanamitindo. Atajiwekea make up za kila aiana japokuwa tayari ana uzuri natural. Atataka avae fasheni mpya mpya zinazotokana kwa kuwa yuko town na mara nyingi hata kama boom haliruhusu kuna wananchi wengi wa kuwapiga mizinga.  Nguo zao wananunulia Mlimani City, Quality Center, Makumbusho, Mwenge kwa White na maeneo mengine kama hayo.  Jinsi wanavyovyaa unaweza ukawaogopa kudhani ni expensive saaaaana.
Binti wa UDOM kwa upande mwingine anavaa kawaida tu. Viatu vyake vya mchomekeo wanavinunua pale SabaSaba lakini waulize wavulana UDOM sasa, watakwambia binti katoka bomba yule si mchezo. Viatu vyao ni bei za kawaida na huvumilia hali zote za hewa. Huwa shopping zao wanafanya Saba Saba. 


Sehemu ya kuangalia movie (cinema)
UDSM huwezi kumpeleka binti kucheka movie room kwako! Sijui eti Hall 3 au ghetto Survey! Utampeleka Suncrest Quality Center au Mlimani City na hapo uweke bajeti ya PopCon na mazagazaga kibao ya kucheki cinema.
Binti wa UDOM wewe tu na laptop yako unamkaribisha chumbani Block 9, 10, etc maeneo ya Haiti mnacheki movie huku mkinywa maji ya kudownload, bites za Discount shop au chai. Umemaliza.
Sehemu ya kukutania (Date location)
Kama unadhani binti wa UDSM utampeleke room yako namba 2409 kule Hall 3 sahau! Kama huna ghetto la ukweli Survey au Sinza au Ubungo Maziwa au unamiliki nyumba kabisa jua imekula kwako. Sehemu ya kukutania lazima iwe ya kueleweka na treatment isomeke vizuri kama misosi iliyosimama, Pizza, Burger, Chicken Chips, etc. Hapo lazima Bamaga upajue vizuri, Mikocheni na Sinza. Kishushio Savanna au Red Bull. Mjomba huna hivyo UDSM utawapata wa kuhesabu kukusikiliza maelezo yako ya kuunga unga.
Binti wa UDOM yeye hata hajali. Wewe tu, uwe kule porini mnapaita Ng’ox au Social Room kwako atakuja. Mtengenezee chai kwa ule mkate wako wa juzi halafu anza kumwaga point zako. Huna haja ya kupajua Area D, Area C wala Lodge za Area A ila ukikosea ukakuta mwenye kaupepo ka jiji lazima kuku wa Club Maisha na 84 ujue bei yake.

Upatikanaji wao (Availability)
Binti wa UDSM atakuona akitaka kukuona si kinyume chake. Ukimpigia simu mkutane atakupa sababu kibao utabaki kichwa kinakuuma ila yeye akikupigia simu mkutane hataki kusikia sababu yako hata moja. Anapenda yeye awe na control.
Binti wa UDOM yeye anaelewa principle ya give and take vizuri sana. Anaelewa mla lazima aliwe na anaelewa ili uhusiano uwepo lazima kila mtu aplay part yake.  Ukimpigia simu baada ya dakika au saa chache utamuona na wanapenda kutembea na wavulana wao campus. Kama unabisha angalia idadi ya mabinti wa UDSM wanaotembea na boys ndani ya campus na wale wa UDOM wanaofanya hivyo ndani ya campus.
Mtazamo wao kuhusu mapenzi (Perception of love)
Binti wa UDSM atakupenda kwa ile ulichona nacho. Kichwa class, una hela au famous. Nje ya hapo ni wa kuhesabu bro.
Binti wa UDOM atakupenda jinsi ulivyo hasa kama shule kasoma Songea huko kwao vijijini chuo katua Dodoma, ila ukikuta ana kahewa ka Dar kidogo lazima utasanda. Yale yale.

Mwandishi wa Makala hii amejitambulisha kuwa ni mhitimu wa Digrii ya Ukandarasi na sasa ni chizi hospitali ya Lutindi Tanga.

SOURCE: ORIGINAL K


Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji betri za simu, na kudai kuwa wa kwanza kutengeneza “the world’s first microbial fuel cells (MFC) powered mobile phone”.
 

Watafiti hao walielezea juu ya ugunduzi wao kupitia jarida la ‘Physical Chemistry Chemical Physics’.
Dr Ioannis Ieropoulos amesema, huo ndio ugunduzi wa kwanza wa kuzalisha nguvu ya umeme kwa kutumia mkojo, na katika majaribio ya utafiti huo wamefanikiwa kuchaji simu ya Samsung.
 

Wanasayansi hao wanaamini kuwa teknolojia yao inaweza kutumika katika mabafu huko mbeleni kwaajili ya kuwashia mashine za kunyolea au kupasha moto maji ya kuoga na kuwasha taa

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, hana mamlaka yoyote ya kukifuta chama hicho.

Mbowe amesema kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwataka wananchi wadai haki zao nje ya utaratibu rasmi, jambo alilosema ni la hatari kwa ustawi wa taifa.

Aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya malori iliyopo katika eneo la Majengo mjini hapa na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa Manispaa ya Songea na mikoa jirani ya Lindi na Mtwara waliofika  kushuhudia uzinduzi wa Kanda ya Kusini ya chama hicho.

Mbowe alisema kuwa binadamu yeyote pale anapodai haki yake, hapaswi kuzuiwa katika mazingira tatanishi, hivyo wanachama wa Chadema wana haki ya msingi ya kujiwekea ulinzi wao (Red Brigade) kama wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walivyojiwekea ulinzi wao kupitia vikundi vya Green Guard na si vinginevyo.

Alisema kuwa suala la Red Brigade siyo geni na wala halijaanzishwa na Mbowe, bali limewekwa bayana kwenye Katiba ya Chadema tangu mwaka 2006 ambapo linasema chama kitajiwekea ulinzi wa mali na viongozi wao, hivyo kuifuta Chadema ni kutafuta machafuko ndani ya nchi.

Mbowe alimtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuona umuhimu wa kuweka miundombinu ya kuwa na amani kwa kusimamia kikamilifu haki kwa vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini badala ya kuwa na upendeleo kwa CCM ambacho kinaonekana kuwa na propaganda nyingi kandamizi za kisiasa.

Alisema kuanzia sasa, Chadema itahakikisha kuwa inakuwa na ulinzi mkali kwa kuweka vikundi vya Red Brigade ambavyo vitakuwapo katika ngazi za serikali za mitaa, vijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa.

Alifafanua kuwa kazi za vikundi hivyo itakuwa ni kulinda usalama wa mali za chama pamoja na viongozi wao.

"Red Brigade ilikuwapo tangu awali isipokuwa kwa hivi sasa kilichofanyika ni kuiongezea uwezo ambao umevifanya vyombo vya dola vishtuke na kuanza kuipigia Chadema kelele ingawa majukumu yake ni yale yale na yanaelekeana na vikundi vya Green Guard vya CCM.

Hata hivyo, Mbowe alisema kuwa vikundi vya  Green Guard vya CCM vimekuwa vikifanya matukio mengi ya kihalifu, lakini Jeshi la Polisi limekuwa likiyafumbia macho.

Alisema anayo mifano ya matukio ya uhalifu ya vikundi vya Green Guard, hakuyataja na kueleza kuwa wahalifu walikamatwa, lakini wakatoroshwa katika mazingira yenye utata.

Kuhusu rasimu ya Katiba, Mbowe amewahimiza wananchi kuwa makini anapoijadili.

Hata hivyo, alisema CCM inataka kuweka taratibu inazozitaka wakati Tume ya Katiba iliandaa vizuri, hivyo Chadema nayo ina mpango wa kuwa na tume yake ya kuijadili rasimu hiyo kwa kuwaelimisha wananchi mambo halisi yanayopaswa kuwapo katika Katiba mpya.      chanzo:chadema blog.

Sultan Kosen MTU MREFU KULIKO WOTE DUNIANI



  
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXrZGSuwtDKT9hSwi9TCpGNDA09HDY-ZAWtzpEI2dAJmAk5iCWvnIxpGFcrjNIZSx2QFKrQqYs-FzgYt0A-uvfgCiGMXZcDmGeMt0SX2ld6GdRzQaiFN485aArUOhBCPmlBkDeM4ikhtM/s320/ch.jpg
Baada ya jana Chidi Benz kuweka wazi kuwa hategemei kumsamehe Baghdad kwa ‘blunder’ aliyoifanya ya kuwashirikisha yeye na Nay wa Mitego bila kuwaambia, mama mzazi wa Baghdad amekuja hadharani na kumuombea msamaha mwanae.
Mama huyo ameongea leo kwenye segment ya 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kuhusu nia yake ya kutaka kumaliza tofauti zilizopo kati ya mwanae na Chidi.

Mama Baghdad amekiri kuwa mwanae hakutumia akili kuchukua uamuzi huo wa kuwashirikisha wasanii wanaofahamika kuwa na uadui mkubwa kimuziki bila kufikiria madhara yake.

Amesema mwanae hakufanya jambo la busara na ndio maana ameamua kumpigia magoti Chidi ili ampe ‘second chance’ mwanae ambaye amejaribu kuomba msamaha bila mafanikio.

255 pia imezungumza na Chidi Benz aliyepo nchini Kenya kwa sasa ambaye amesema hawezi kukataa wito wa mama yake na Baghdad kwakuwa ni kama mama yake pia na amekubali kuja kukutana naye akirejea nchini.

Jana wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya, Chidi alisema kamwe hatokuja kumsamehe Baghdad. 

Source:Mambo Mseto {Radio Citizen},Kenya




Rapcellency, Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kwakuwa anaamini hakuna alichomkosea na ni jambo la kitoto.
 Akiongea jana  mchana kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen, kinachoendeshwa Mzazi Willy M. Tuva, Prezzo amesema Diamond ndiye aliyemchokoza baada ya wasanii hao kutumbuiza mwanzoni mwa mwezi huu kwenye tamasha la Matumaini.

 Prezzo anadai aligundua kuwa Diamond alimponda kwenye magazeti ya Tanzania kuwa hamwezi kwa lolote kwenye muziki.

“Mimi sipendi kuwa na adui kwa sababu muziki unafaa kuleta muungano, sa me nikashangaa mbona huyu brother ananiingilia na huku sikumbuki kumkosea wala hatujawai kukutana ana kwa ana,” alisema Prezzo.
 
“Mtu yeyote anamjua Prezzo ni kama rattle snake, ukimchokoza you have to get prepared to be bitten.”
 Rapper huyo aliendelea kudai kuwa alimpigia simu Diamond lakini hakupokea na ndio maana aliamua kumdiss kwenye Twitter.
  “Jamaa hakupokea simu nikaona ah! Basi liwalo na liwe, nikadecide ku-air my views.”
Hata hivyo Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kama anavyomtaka afanye.
 
 “Unaona kwa saa hizi akianza kusema aende kwa Twitter aniombe msamaha, maisha huwa hayaendi hivo…kwa hivyo vitu vingine naona ni kama ni utoto unaingilia kati, kwani yeye kusema niombe msamaha kwa Twitter….niombe msamaha kwa kosa gani? Kusema ukweli,unajua mimini msema ukweli, mimi kuomba msamaha kwa Twitter naona kidogo ni utoto.”
Hata hivyo Prezzo amesema hataki beef na Diamond kwasababu anamheshimu na amemshukuru Willy Tuva kwa kujaribu kuwasuluhisha.

Kapteni John Kivunge, Wafanyakazi wa Tanzania Afisa Joc, wasomaji mpango wa sherehe fupi.
 
Sala kutoka kwa mchungaji.
 
Maombi kutoka kwa Imamu kwa walinzi wa amani wa waasi.

 .. 
Kijeshi salute kama pete 'Last Post' nje na Nigbatt kwa heshima ya mashujaa imeanguka
Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz