Battlefield 3 multiplayer review
Lorem ipsum dolor sit amet, conscur adisng elit, sed do eiusmod tempor iniunt ut labore et dolore mana aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exetation ullco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo coequat. Duis aute irure dolor
A Bathing Ape 2011 Winter Collection
Lorem ipsum dolor sit amet, conscur adisng elit, sed do eiusmod tempor iniunt ut labore et dolore mana aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exetation ullco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo coequat. Duis aute irure dolor
Diablo 3 beta gameplay video
Lorem ipsum dolor sit amet, conscur adisng elit, sed do eiusmod tempor iniunt ut labore et dolore mana aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exetation ullco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo coequat. Duis aute irure dolor
Killer Elite movie review
Lorem ipsum dolor sit amet, conscur adisng elit, sed do eiusmod tempor iniunt ut labore et dolore mana aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exetation ullco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo coequat. Duis aute irure dolor
![]() |
Watafiti hao walielezea juu ya ugunduzi wao kupitia jarida la ‘Physical Chemistry Chemical Physics’.

Wanasayansi hao wanaamini kuwa teknolojia yao inaweza kutumika katika mabafu huko mbeleni kwaajili ya kuwashia mashine za kunyolea au kupasha moto maji ya kuoga na kuwasha taa
Mbowe amesema kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwataka wananchi wadai haki zao nje ya utaratibu rasmi, jambo alilosema ni la hatari kwa ustawi wa taifa.
Aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya malori iliyopo katika eneo la Majengo mjini hapa na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa Manispaa ya Songea na mikoa jirani ya Lindi na Mtwara waliofika kushuhudia uzinduzi wa Kanda ya Kusini ya chama hicho.
Mbowe alisema kuwa binadamu yeyote pale anapodai haki yake, hapaswi kuzuiwa katika mazingira tatanishi, hivyo wanachama wa Chadema wana haki ya msingi ya kujiwekea ulinzi wao (Red Brigade) kama wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walivyojiwekea ulinzi wao kupitia vikundi vya Green Guard na si vinginevyo.
Alisema kuwa suala la Red Brigade siyo geni na wala halijaanzishwa na Mbowe, bali limewekwa bayana kwenye Katiba ya Chadema tangu mwaka 2006 ambapo linasema chama kitajiwekea ulinzi wa mali na viongozi wao, hivyo kuifuta Chadema ni kutafuta machafuko ndani ya nchi.
Mbowe alimtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuona umuhimu wa kuweka miundombinu ya kuwa na amani kwa kusimamia kikamilifu haki kwa vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini badala ya kuwa na upendeleo kwa CCM ambacho kinaonekana kuwa na propaganda nyingi kandamizi za kisiasa.
Alisema kuanzia sasa, Chadema itahakikisha kuwa inakuwa na ulinzi mkali kwa kuweka vikundi vya Red Brigade ambavyo vitakuwapo katika ngazi za serikali za mitaa, vijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa.
Alifafanua kuwa kazi za vikundi hivyo itakuwa ni kulinda usalama wa mali za chama pamoja na viongozi wao.
"Red Brigade ilikuwapo tangu awali isipokuwa kwa hivi sasa kilichofanyika ni kuiongezea uwezo ambao umevifanya vyombo vya dola vishtuke na kuanza kuipigia Chadema kelele ingawa majukumu yake ni yale yale na yanaelekeana na vikundi vya Green Guard vya CCM.
Hata hivyo, Mbowe alisema kuwa vikundi vya Green Guard vya CCM vimekuwa vikifanya matukio mengi ya kihalifu, lakini Jeshi la Polisi limekuwa likiyafumbia macho.
Alisema anayo mifano ya matukio ya uhalifu ya vikundi vya Green Guard, hakuyataja na kueleza kuwa wahalifu walikamatwa, lakini wakatoroshwa katika mazingira yenye utata.
Kuhusu rasimu ya Katiba, Mbowe amewahimiza wananchi kuwa makini anapoijadili.
Hata hivyo, alisema CCM inataka kuweka taratibu inazozitaka wakati Tume ya Katiba iliandaa vizuri, hivyo Chadema nayo ina mpango wa kuwa na tume yake ya kuijadili rasimu hiyo kwa kuwaelimisha wananchi mambo halisi yanayopaswa kuwapo katika Katiba mpya. chanzo:chadema blog.
Mama huyo ameongea leo kwenye segment ya 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kuhusu nia yake ya kutaka kumaliza tofauti zilizopo kati ya mwanae na Chidi.
Mama Baghdad amekiri kuwa mwanae hakutumia akili kuchukua uamuzi huo wa kuwashirikisha wasanii wanaofahamika kuwa na uadui mkubwa kimuziki bila kufikiria madhara yake.
Amesema mwanae hakufanya jambo la busara na ndio maana ameamua kumpigia magoti Chidi ili ampe ‘second chance’ mwanae ambaye amejaribu kuomba msamaha bila mafanikio.
255 pia imezungumza na Chidi Benz aliyepo nchini Kenya kwa sasa ambaye amesema hawezi kukataa wito wa mama yake na Baghdad kwakuwa ni kama mama yake pia na amekubali kuja kukutana naye akirejea nchini.
Jana wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya, Chidi alisema kamwe hatokuja kumsamehe Baghdad.
Source:Mambo Mseto {Radio Citizen},Kenya
![]() |
Rapcellency, Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kwakuwa anaamini hakuna alichomkosea na ni jambo la kitoto. Akiongea jana mchana kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen, kinachoendeshwa Mzazi Willy M. Tuva, Prezzo amesema Diamond ndiye aliyemchokoza baada ya wasanii hao kutumbuiza mwanzoni mwa mwezi huu kwenye tamasha la Matumaini.
Prezzo anadai aligundua kuwa Diamond alimponda kwenye magazeti ya Tanzania kuwa hamwezi kwa lolote kwenye muziki.
“Mimi sipendi kuwa na adui kwa sababu muziki unafaa kuleta muungano, sa me nikashangaa mbona huyu brother ananiingilia na huku sikumbuki kumkosea wala hatujawai kukutana ana kwa ana,” alisema Prezzo.
“Mtu yeyote anamjua Prezzo ni kama rattle snake, ukimchokoza you have to get prepared to be bitten.” Rapper huyo aliendelea kudai kuwa alimpigia simu Diamond lakini hakupokea na ndio maana aliamua kumdiss kwenye Twitter.
“Jamaa hakupokea simu nikaona ah! Basi liwalo na liwe, nikadecide ku-air my views.”
Hata hivyo Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kama anavyomtaka afanye.
“Unaona kwa saa hizi akianza kusema aende kwa Twitter aniombe msamaha, maisha huwa hayaendi hivo…kwa hivyo vitu vingine naona ni kama ni utoto unaingilia kati, kwani yeye kusema niombe msamaha kwa Twitter….niombe msamaha kwa kosa gani? Kusema ukweli,unajua mimini msema ukweli, mimi kuomba msamaha kwa Twitter naona kidogo ni utoto.”
Hata hivyo Prezzo amesema hataki beef na Diamond kwasababu anamheshimu na amemshukuru Willy Tuva kwa kujaribu kuwasuluhisha.












