Vienna, Austria ni nyumbani mpya ya kwanza ya Dunia ya kimataifa shule kutumiwa ngono, ambayo inadai kuwafundisha wanafunzi wake jinsi ya kuwa bora wapenzi.
"Mikono" silabasi gharama wanafunzi wanafunzi baridi £ 1,400 kwa kila mrefu na kuona wanaoishi katika mabweni mchanganyiko ngono, ambapo, wanatarajiwa kufanya mazoezi ya kazi zao za nyumbani. Hmmm, mimi ajabu ni aina gani ya kazi ya nyumbani kutumika kujamiiana kuwa ni!
Ylva-Maria Thompson, Sweden mzaliwa headmistress wa chuo anasema kuwa msingi yao elimu si kinadharia, lakini sana vitendo.
"Kimapenzi nafasi, caressing mbinu, anatomical makala. Na sisi kufundisha mikono juu ya watu, "anaelezea Thompson.
Basi hebu kupata haki hii, kulipa na kukaa katika chuo ambapo una mapenzi na wanafunzi wengine na labda hata walimu wako. Hii tu inaonekana kama nyumba halali maalumu kwa ajili hiyona ni kwa watu wazima-tu- bandari ngono!
Swali: Je ungeweza kujiunga na SHULE KAMA HII


 

 

 

 

 

 

 

                                                                                                                                                                                                                        

Sasa ni kati ya Chama cha Tiba Asili (ATME) na  TDFA.  ATME kinadai hayana madhara wagonjwa wake wameyatumia kwa zaidi ya miaka 20.

Dar es Salaam. Mratibu wa Chama cha Watabibu wa Dawa za Asili Tanzania (ATME), Boniventure Mwalongo amesema taarifa zilizotolewa hivi karibuni na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TDFA) kuhusu matumizi ya mafuta ya ubuyu zinaweza kuleta madhara kwa jamii kwa sababu watu wengi wamekuwa wakiyatumia.

Akitolea mfano watumiaji wakubwa  wa mafuta hayo, Mwalongo alisema, wenye magonjwa kama ya moyo na wanaoishi na Virusi vya Ukimwi wamekuwa wakiyatumia mafuta hayo kwa muda mrefu na kudai yamewasaidia.

Mwalongo ameyasema hayo jana baada ya hivi karibuni kuibuka utata kuhusu ubora na usalama wa mafuta hayo na kudai kuwa wao kama ATME walianza kuyatumia kama dawa kwa wateja wao siku nyingi na hawajawahi kupata malalamiko yoyote na kuwahakikishia watumiaji kuwa hayana madhara.

 “Yametumika kwa zaidi ya miaka 20 na sisi tunazo kumbukumbu za wagonjwa tuliowapa mafuta hayo kama dawa na hatujawahi kupata ripoti yoyote ya madhara kwa wale waliotumia,” alisema Mwalongo.   TFDA ilitoa taarifa kwamba mafuta hayo hayafai kwa matumizi ya binadamu kwa sababu yana kiwango kikubwa cha tindikali ya mafuta aina ya cyclopropenoic fatty acids.

  Katika taarifa ya TFDA iliyotolewa juma lililopita ilisema athari zinazoweza kutokea kutokana na matumizi ya mafuta hayo ni pamoja na kuathiri vimeng’enyo vinavyosaidia katika uchakataji wa tindikali za mafuta mwilini.

  Pia ilisema ili yaweze kukidhi vigezo vya ubora na usalama ni lazima yafanyiwe usafishaji wakati wa usindikaji na kwamba kwa sasa nchini hakuna aina ya usindikaji unaofanyika wenye uwezo wa kuondoa tindikali hiyo ya cyclopropenoic fatty acids katika mafuta ya mbegu za ubuyu.

 Hata hivyo Mwalongo alikemea usambazaji holela wa mafuta hayo hasa baada ya kubainika kuwa yanatibu maradhi mbalimbali ambapo baadhi ya wajasiriamali wamekuwa wakiyasambaza wakati siyo wataalamu wa tiba asili.

  Mratibu huyo alizishauri mamlaka zinazohusika na suala zima la afya ya binadamu nchini kutoa majibu yatakayosaidia kuondoa mgawanyiko uliopo sasa kutokana na mafuta hayo badala ya kutoa taarifa za kutisha.

   Hata hivyo alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Tiba Asili kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Paul Mhame, alisema hawana taarifa zozote kama kuna tafiti zimefanyika kuhusiana na matumizi ya mafuta hayo

 

 

 

 

 

 




 

 

 

 

 

 



Utafiti unaonyesha  vijana wanaojihusisha na vitendo hivyo wanatolewa vijijini
Dar es Salaam.  Asilimia 65 ya vijana kata za Buguruni na Vingunguti wapo hatarini kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutokana na kujihusisha na biashara ya ushoga na uchangudoa.
Katika utafiti uliofanywa na Shirika la Ushauri kwa Familia (CAFLO) mwishoni mwa mwaka jana, uneonyesha idadi kubwa ya vijana hao ni wenye umri kuanzia miaka 12 na kuendelea.
Akizungumza kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana na watu wanaoishi na VVU kutoka maeneo hayo juzi, Mwenyekiti wa shirika hilo, Mariam Mlugu, alisema idadi kubwa ya vijana hao ni wale waliochukuliwa kutoka mikoani kufanya kazi za ndani.
Mlugu alisema baada ya kufika Dar es Salaam, vijana hao wamejikuta wakiingia kwenye biashara hizo kutokana na unyanyasaji na ujira mdogo.
Alisema baada ya utafiti huo waliwasiliana na Kamati ya Ukimwi Manispaa ya Ilala ambayo ilikubali kuliwezesha shirika hilo kutoa mafunzo kwa vijana na wanaoishi na VVU, ili wabuni na kutafuta fursa mbalimbali kujiletea maendeleo.
Pia, Mlugu alisema baadhi ya  familia na jamii zimekuwa zikikosa fursa kufanya shughuli halali na kuamua kujiingiza kwenye kazi hatarishi, kama  biashara ya ngono na mapenzi ya jinsia moja kwa lengo la kujipatia kipato.
Awali, Mkurugenzi wa utawala wa shirika hilo, Dennis Mikongoti, alisema mafunzo hayo yana lengo la kuwajengea uwezo watu wanaoishi na VVU na Ukimwi na ambao wapo hatarini kupata magonjwa hayo,  ili wapambane na umaskini wa kipato ambao ndiyo unachangia kwa kasi maambukizi hayo. Naye
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Ilala, Malcela Msawanga, aliwaasa washiriki hao kutumia mafunzo hayo kuwaelimisha wenzao ambao hawakupata fursa hiyo.

 Mwenyekiti wa Chama Cha Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema, pichani, amechaguliwa na mkutano Mkuu wa Kituo cha Demokrasia nchini (TCD), kuwa Mwenyekiti mpya atakayekiongoza kwa mwaka mmoja.

Uchaguzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki na wajumbe wapatao 25 ambapo Mrema alipita bila kupingwa na kupewa nafasi hiyo baada ya mtangulizi wake, James Mbatia, kutoka NCCR-Mageuzi kumaliza muda wake.

Katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo, alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa kituo hicho.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuchaguliwa, Mrema alisema amefarijika kuwa bosi katika kituo hicho kinachoundwa na vyama sita vyenye wawakilishi bungeni kikiwamo Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo, TLP, Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na UDP.

Aidha, Mrema alisema yeye na viongozi wenzake wataendeleza yale yote yaliyofanywa na watangulizi wao kwa lengo moja la kujenga siyo kubomoa.





Stori: Mwandishi WetuHAKUNA sababu ya kumkamata ‘mchawi’  kwenye skendo ya Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ kudaiwa kukamatwa na madawa ya  kulevya nchini Afrika Kusini wakati ukweli upo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Watu mbalimbali ambao wamesoma sakata hili kwenye vyombo vya habari, walitoa maoni yao wakisema kuwa watu wanaotakiwa kuwajibishwa ni waliokuwa uwanjani hapo siku Masogange aliposafiri na kuruhusu mizigo ya mrembo huyo na mdogo wake, Melisa Edward ipite bila ukaguzi makini.
“Kuna uwezekano kabisa wa kuwajua watu hao,” alisema msomaji wetu, Mbande Kinaka, mkazi wa Kariakoo, Dar.
Risasi Jumamosi lilimtafuta Mkuu Kitengo cha Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Kamanda Godfrey Nzowa, alipopatikana na kuulizwa namna ya kuwabaini waliomruhusu Masogange akapenya na mzigo airport, alisema lazima watawapata.


Taarifa tulizozipata zinasema Agnes na mdogo wake Melisa Edward  waliondoka nchini Julai 5, mwaka huu kwenda Afrika Kusini.

KAMANDA MPINGA AFUNGA MAFUNZO YA MADEREVA 278 WA PIKIPIKI ZA MIGUU MIWILI (BODABODA) GONGOLAMBOTO JIJINI DAR

 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP. Mohammed R. Mpinga  akiongea na kuwaasa  madereva wa Bodaboda wakati wa kufunga mafunzo hayo. Kushoto kwa Kamanda ni Rais wa AAT Mr Nizan Jivan, CEO wa AAT Mr Yusuf Aghor na Mweka hazina wa AAT Mr Pepe.
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP Mohammed  Mpinga  akikabidhi cheti kwa mhitimu Mwanamke aliyehitimu  mafunzo ya Elimu ya Usalama Barabarani yaliyotolewa kwa madereva wa Bodaboda Dsm na Kikosi cha Usalama Barbarani kwa kushirikiana na AAT  (Automobile Association of Tanzania) kwa ufadhili wa chama cha mashindano ya Magari Duniani (FIA) wakati ufugaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika Gongolamboto 10/07/2013. Anayeangalia ni Rais wa AAT Mr Nizan Jivan
Mr Nizan Jivan Rais wa Automobile Association of Tanzania (AAT) akiongea na madereva wa Bodaboda wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika Gongolamboto – Dar es salaam 10/07/2013. Kulia ni Mr Yusuf Aghor CEO wa AAT na kushoto ni ASP Swai wa Makao Makuu ya Traffic Dsm.
 Mr Nizan Jivan Rais wa Automobile Association of Tanzania (AAT) akipokea zawadi maalum kutoka kwa wahitimu wa Mafunzo ya  dereva wa BODABODA mkoani Dar es Salaam kama shukrani yao ya pekee kwa kudhamini mafunzo haya bure kwa madereva wa Bodaboda, ufugaji wa mafunzo ya elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda ulifanyika Gongolamboto Dsm  tarehe 10/07/2013.
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP Mohammed R.  Mpinga  (kushoto) akikabidhiwa Tuzo maalum ya ushiriki wake katika kusimamia mafunzo ya Bodaboda mkoa wa Dar es Salaam. Tuzo hiyo alikabidhiwa  na Rais wa Automobile Association of Tanzania (AAT) Mr Nizani Jivan wakati  wa ufungaji wa mafunzo ya elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda tarehe 10/07/2013 Gongolamboto – Dar es salaam. 
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP Mohammed   Mpinga  akiwa katika picha ya pamoja na  Rais wa Automobile Association of Tanzania (AAT) na wadau mbalimbali waliohudhuria katika ufugaji wa mafunzo ya elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda, tarehe 10/07/2013  Gongolamboto - Dsm. 
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP Mohammed R.  Mpinga  akikabidhi cheti kwa mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda katika ufugaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 10/07/2013  Gongolamboto – Dsm.
 Madereva Bodaboda wa mkoa wa Dar es Salaam wakipokea kiapo chao cha utii kuashiria kuwa mafunzo ya Elimu ya Usalama Barabarani waliyoyapata darasani sasa watayafanya kwa vitendo wawapo katika kazi zao za usafirishaji wa abiria katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam. Kiapo hiki kilifanyika mbele ya Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani DCP Mpinga wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo kwa madereva wa Bodaboda Gongolamboto 10/07/2013.
Sehemu ya Madereva Bodaboda wa mkoa wa Dar es Salaam wakimsikiliza Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani pichani hayupo wakati wa ufungaji wa mafunzo ya Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda. Ufugaji wa mafunzo hayo ulifanyika Gongolamboto tarehe


Mwanafunzi wa Chuo cha Ufundi (Veta) mkoani Dodoma, Taliki Juma, (22) amefariki dunia baada ya kujilipua kwa kutumia mafuta ya petroli na kujeruhi wengine nane.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 10.30 jioni Nzuguni eneo la Machaka, nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma Mjini.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Suzan Kaganda, jana alisema Taliki alijilipua katika saluni inayomilikiwa na Irene Mapunda inayojulikana kwa jina la Tonny Hair Dressing Saloon.

Alisema mwanafunzi huyo aliyekuwa akisomea fani ya ufundi magari, alienda kununua Petroli lita tano katika kituo cha Mafuta cha Nanenane na kuimwaga ndani ya chumba cha  Saluni ya Irene.

Watu waliokuwa karibu naye walijaribu kumsihi asijilipue lakini hawakufanikiwa kwani Taliki aliwasha kibiriti ndani ya saluni hiyo na kusababisha moto mkubwa kulipuka ambao uliwaunguza wote waliokuwa karibu naye pamoja na mali zote zilizokuwa ndani ya Saluni hiyo,” alisema.

Aliwataja majeruhi hao kuwa ni Mugina Hussein (32), Swaibu Kassimu (20), Easte Silau (30) na Fredrick Gabriel (21), wote wafanyabiashara na wakazi wa Nzuguni.


Wengine ni mwanafunzi wa darasa la nne Benson Mushi (11), Japhet Japhet (18), Meshack John (18) na mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya City, Shaban Pili (20).

Alisema majeruhi wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambapo nane wamelazwa wodi namba moja ya wanaume na mmoja amelazwa wodi namba 10 ya wanawake.

Kaganda alisema tathimini ya hasara iliyosababishwa na moto huo bado haijafahamika.

Aidha, alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa, chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi.

Hata hivyo, alisema  Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kina juu ya tukio hili.


MUUGUZI WA ZAMU

Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Magreth Maki, alisema kuwa Taliki alifariki jana katika hospitali hiyo kutokana na majeraha makubwa aliyopata wakati wa tukio hilo.

Hata hivyo, alisema hali ya majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wanaendelea vizuri isipokuwa mmoja ambaye bado hali yake si nzuri.

“Bado wanaendelea kutibiwa vidonda walivyovipata kutokana na tukio hilo, hali yao inaendelea vizuri isipokuwa mmoja ambaye hali yake ni serious (mbaya),
“alisema Muuguzi huyo wa zamu.
 

Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya City mjini Dodoma, Shaban Pili (18), akiwa katika wodi namba moja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. Shaban ni mmoja wa majeruhi walioungua moto katika tukio la mwanfunzi wa Chuo cha Veta Dodoma kujilipua na kufariki Dunia lilitokea Nzuguni eneo la Machaka nje kidogo ya mji wa Dodoma.
MAJERUHI WANENA
Akizungumza na NIPASHE, baba mzazi wa Benson Mushi, Dickson Mushi, alisema kuwa mwanae alikumbana na mkasa huo alipokwenda kupeleka nguo zake kwa ajili ya kunyoosha

“Mwanangu alikwenda karibu na saluni hiyo kwa ajili ya kwenda kunyoosha nguo zake ndipo alipokutana na mkasa huu. Amekuwa na kawaida ya kwenda kuonyoosha karibu na saluni hiyo,”
alisema Mushi alipokuwa akizungumza na gazeti hili nje ya wodi.

Kwa upande wake, majeruhi mwingine Shaban Pili, alisema alikumbwa na mkasa huo katika jitihada za kumuokoa marehemu baada ya kusikia kelele za kuomba msaada kutoka kwa wafanyabiashara waliopo jirani na saluni hiyo.

“Tuliangaika kuvuta mlango wa saluni na tukafanikiwa, tulipomuuliza kulikoni amejimwagia petroli, alitujibu kuwa tumwache lakini ghafla aliwasha kiberiti na kujilipua,”alisema na kuosha mkono aliungua sana wakati alipokuwa akimvuta marehemu nje ya saluni hiyo.

Naye majeruhi Meshack John, alisema alikuwa amekaa karibu na saluni hiyo, ndipo alipokuja marehemu (mtoto wa baba yake mdogo) na kumuomba ampatie Sh. 15,000.

“Nilimuuliza ya nini? Akanijibu kuwa baba kanituma (baba yake mdogo ambaye ni mmliki wa bucha analouza nyama katika eneo la Nzuguni), nikakataa na kuwaomba ushauri wenzangu kama nimpatie ama la,”alisema.

Hata hivyo, baada ya mashauriano ya muda mrefu akaamua kumpatia kiasi hicho cha fedha na akaondoka zake na kwenda kununua mafuta ya petroli lita tano.

Alisema baadaye alirejea na lita tano za mafuta na kisha kujifungia ndani ya saluni kabla ya kujimwagia.

“Akajimwagia, mama mmoja naye amelazwa hapa hapa, akasema Taliki anajiwasha huko moto naona mafuta yanatiririka huku nje,”alisema.

Alisema hali hiyo ilisababisha wasogeze mlango wa saluni na kabla hawajachukua hatua moto ukaanza kuwaka.
 
“Tulikuwa majeruhi tisa lakini mwenzetu Taliki alifariki dunia leo asubuhi kwa kuwa yeye alijimwagia mafuta kabla kujilipua moto
,”alisema.

Kwa upande wa chanzo la tukio hilo, alisema kuwa marehemu alikuwa na ugomvi na wenzake ambao aliwashutumu kwamba wanamtangazia kuwa anauhusiano wa kimapenzi na mmiliki wa saluni hiyo (Irene).

“Walikuwa wanamtangazia kuwa amekuwa akimhonga (mmiliki wa saluni) pesa…Ijumaa walipigana sana  na wenzake hadi alirudi nyumbani kuchukua panga akitaka kuja kuwakatakata wenzake akidai kwanini wampakazie jambo ambalo halina ukweli,alisema.

Majeruhi huyo alisema ilimbidi kwenda kuamulia ugomvi huo na ukaisha lakini alishangaa tena juzi marehemu aliamua kuchukua uamuzi huo.

Naye Silau, aliyelazwa wodi namba 10, alisema  alikuwa akifanya biashara karibu na saluni hiyo ndipo moto ulipomrukia na kumuunguza mikononi.

“Mimi nilisikia harufu ya mafuta ya petroli na kuwaambia wenzangu kuwa nasikia harufu katika saluni hiyo lakini sikusogea karibu,”alisema Silau.
 
MASHUHUDA
Mashuhuda wa tukio hilo ambao hawakutaka majina yao kuandikwa gazetini walisema kuwa marehemu huyo alipelekwa hospitali akiwa ameungua vibaya kiasi cha ngozi yote kuchunika.

“Marehemu alikuwa akilalamika maumivu, akisema  anatamani kufa mapema maana maumivu ni makali sana,”alisema mmoja wa shuhuda wa tukio hilo
Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz