TAMATI YA BONANZA A.J.T.C. KUJULIKANA LEO



Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wanatarajiwa kumaliza bonanza liloanza siku ya jumatano chuoni hapo 
Akizungumza na BLog hii kwa nyakati tofauti mwalimu wa michezo chuoni hapo amesema kuwa mashindano yaliyoandaliwa na kamati ya michezo yana malizika leo.
Baadhi ya michezo iliyokuwamo ni mpira wa miguu,netball,kucheza karata,kula,kuzunguka viti,kucheza draft na mingine mingi.Alisema lengo ni kutafuta timu bora ya chuo pamoja na kuwafanya wanafunzi kuwa vizuri kiafya na kiakili kwani michezo hujenga mwili kwa kufanya mazoezi.
Pia waalimu wa chuo hicho walihusishwa kwenye mashindano hayo kwa kupewa dhamana ya kuwa marefa kwenye mpira wa miguu pamoja na netball.
Wanafunzi wa chuo hicho walionyesha ushirikiano mzuri kwa kuwashabikia wenzao walipokuwa wakicheza.
Zawadi za washindi wote kwa ujumla zitatolewa leo chuoni hapo baada ya kumalzika kwa michezo yote...

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz