ROSE NDAUKA SASA KUZAA BILA NDOA,MAMA YAKE AGOMA...


0 comments:

Serikali yafungia magazeti ya Mwananchi, Mtanzania


Mkurugenzi wa Habari (MAELEZO), Assah Mwambene amethibitisha jana kuwa serikali imeyafungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania kwa kile ilichokiita "kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama."

0 comments:

AIBU: WANADAMU TUNAELEKEA WAPI? HEBU CHEKI SHOGA ALIVYO UMBULIWA MTAANI.... Kwa kuvuliwa nguo na kutembezwa uchi..TAZAMA VIDEO HAPA

 
SHOGA moja nchini Nigeria limejikuta likiangukia mikononi mwa polisi wa nchini hiyo baada ya kujifanya ni DEMU... 

0 comments:

MALI KWA MALI: BABA MZAZI AMBAKA MWANAE KWA MIEZI 9..... DU! BALAA HILI...!!! TAZAMA PICHA NA HABARI HAPA


KWELI dunia haina huruma! Binti wa umri wa miaka 15 tunayemtambulisha kwa jina moja tu la Zaina, mkazi wa Kimara jijini Dar ameamua kufunguka na kusimulia jinsi alivyokuwa akibakwa na baba yake mzazi aliyemtaja kwa jina moja la Mohamed,

0 comments:

HEBU CHEKI MAJINA YA ASILI YA BAADHI YA MASTAR WA BONGO MOVIES HAPA



KWA kawaida binadamu yeyote huzaliwa na kubatizwa jina ambalo hulitumia katika masomo na hata kazi yake.
Tofauti na ilivyo katika fani nyingine, wasanii wamekuwa wakijibatiza majina ya ziada (A.k.a). Mbaya zaidi, majina hayo huwa yanaanza kama utani lakini inafika wakati msanii husika

analizoea jina hilo jipya na kulifanya kuwa kama rasmi. Leo Amani linakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao majina waliyopewa na wazazi wao ‘yamekufa’, hawayatumii kabisa: LULU

Jina lake halisi ni Elizabeth Michael, Lulu lilizoeleka kupitia tasnia ya uigizaji. Alianza kulitumia wakati alipojiunga na Kundi la Sanaa la Kaole.

Hadi leo hii, siyo rahisi kabisa mtu kutokea na kumuita jina la Elizabeth, wengi wanamfahamu kwa jina la Lulu.
RAY
Ray ndiyo jina ambalo limezoeleka na wengi. Vincent Kigosi alilopewa na wazazi wake ni kama limekufa. Kwa zaidi ya miaka kumi sasa tangu alipokuwa kwenye Kundi la Sanaa la Kaole hadi sasa.
Jina la Ray ndiyo watu wanalolifahamu zaidi ingawa hivi karibuni baadhi ya wasanii wenzake wamekuwa wakijaribu kumuita Vincent ili kurudisha uhai wa jina hilo.






JOHARI
Jina lake halisi ni Blandina Chagula. Johari lilizaliwa kwenye Tamthiliya iliyobeba taito ya jina hilo. Akiwa katika Kundi la Kaole, alianza kujiita Blandy, baadaye alibadilisha jina hilo na kuwa Johari walipoingiza tamthiliya hiyo ambayo pia ilizaa filamu.




“Kuna wakati huwa najuta kutumia jina la a.k.a ambalo limefunika kabisa jina langu la asili,” anasema Johari.

DK. CHENI
Ameanza gemu kitambo, tangu Kundi la Splended. Jina alilopewa na wazazi wake ni Mahsein Awadhi, kwa sasa limekufa. Hakuna anayelitumia, hata yeye mwenyewe.
Jina hilo lilizaliwa baada ya mazoea yake ya kupenda kuvaa cheni kubwa kwenye michezo iliyokuwa ikirushwa Runingani, kwa sasa wengi wanashindwa hata kulitamka jina lake. ODAMA
Jina lake halisi ni Jenniffer Kyaka, limekufa kabisa kwa sasa. Wengi wanamfahamu kama Odama jina ambalo alilipata kwenye filamu iliyoitwa Odama miaka sita iliyopita
Tangu ilipotoka filamu hiyo hadi leo, jina la Odama limegeuka kuwa ndiyo la asili.
BATULI
Jina alilopewa na wazazi wake ni Yobnesh Yusuf lakini wengi hawalijui. Alianzia kuigiza katika Kundi la Kaole. Alianza kujiita Nesh, baadaye akabadilisha na kujiita Batuli baada ya kucheza filamu ya ‘Fake Smile’ ya marehemu Steven Kanumba.
Toka hapo, watu wote wakamfahamu kupitia jina la Batuli, wachache sana wanaolijua jina la Yobnesh, zaidi ni ndugu zake wa karibu.
JB
Majina mengi ya a.k.a ameitwa. Aliitwa Bonge la Bwana, Mtumishi, Eric Ford na mwisho jina la JB likasimama katika akili za watu.
Mwenyewe anasema jina la JB analipenda sana, kuna wakati hata yeye huwa anasahau kabisa kama anaitwa Jacob.



NORA
Jina lake halisi ni Nuru Nassoro. Takriban miaka kumi iliyopita baada ya kujiunga na Kundi la Kaole, jina la Nuru limekufa kabisa.
Familia yake nzima wanatumia jina la Nora na si Nuru tena, amelikubali na analipenda kutoka moyoni mwake.

RICHIE RICHIE
Huyu naye ni msanii wa muda mrefu, jina lake halisi ni Single Mtambalike. Wengi hawalifahamu jina lake halisi.
Wanamuita Richie Richie utadhani ndiyo alilopewa na wazazi wake, jina hilo alipewa takriban miaka kumi na tano iliyopita akiwa na Kundi la Nyota Ensembles.

CATHY
Huyu anaitwa Sabrina Rupia, Cathy lilikuja katika michezo kipindi hicho akiwa katika Kundi la Nyota Ensembles. Limeendelezwa hadi leo na kipo kizazi ambacho hakilifahamu kabisa jina la Sabrina zaidi ya Cathy

0 comments:

RISASI ZILIZOFYATULIWA OVYO NA WANAMGAMBO WA AL-SHABAAB ZILIWALENGA NA KUZITOA ROHO ZA WATU MAARUFU BAADA YA KUVAMIA JUMBA LA MADUKA LA WESTGATE MALL NCHINI KENY

HAWA NDIO WATU MAARUFU WALIOFARIKI KWENYE WESTGATE MALL NCHINI KENYA.KOFI AWOONOR.

0 comments:

DIAMOND PLATNUMZ KUJING'ARISHA NA GRAMU 87.97 ZA GOLD SHINGONI KWAKE...!!HII NI BAADA YA SHOW YAKE ALIOFANYA JANA HUKO NCHINI MALASIA

0 comments:

TANZANIA YATENGWA RASMI NA EAC.....!!


HATIMAYE Tanzania imewekwa kando rasmi na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), katika kuunda Shirikisho la Kisiasa litakaloziongoza nchi hizo.

0 comments:

UJUMBE ALIYO ANDIKA AGNESS MASOGANGE FACEBOOK WAZUA MASWALI..JE KAACHIWA HURU?

Hii ni post aliyoiweka Agnes Masogange kwenye ukurasa wake wa FB na imeanza kusambaa kwa kasi kupitia wasanii mbalimbali na mm nimeinasa kwa boss ngasa blog:
Je yawezekana wametoka?Au ndio zile fununu kuwa wanapiganiwa kesi yao irejee nchini?
Tungoje kama ni kweli ama uzushi

0 comments:

SHAHIDI AFARIKI GHAFLA MAHAKAMANI WAKATI AKITOA USHAHIDI HUKO MKOANI MARA...!!

Katika hali isiyo ya kawaida, mkazi wa Kijiji cha Lorwe Kata ya Nyahongo Shirati, wilayani Rorya, mkoani Mara, Charles Warito (38), ambaye ni shahidi wa  mlalamikaji  katika Kesi ya kudhuru mwili kwa kujeruhiwa vibaya kwa kukatwa mkono na kusababisha ulemavu amefariki dunia, wakati akitoa ushahidi.

0 comments:

HATIMAYE MWANADADA JACQUELINE WOLPER AVURUGA UTARATIBU KATIKA SHEREHE MSANII MWENZAKE...! CHEKI HAPA


SURA ya mauzo kwenye sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper amesababisha usumbufu mkubwa kwa waalikwa wa bethidei ya chipukizi wa filamu, Mumy Mushi.

0 comments:

CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA (AJTC) KUPATA SEMINA YA UJASIRIAMALI KESHO

 
Mkurugenzi wa mafunzo ya chuo cha uandishi wa habari na utangazaj Arusha(AJTC) Aliyevaa koti jeupe akiwa na baadhi ya waalimu wa chuo hicho akisikiliza mada. 

Jumla ya wanachuo 227 wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wanatarajiwa kushiriki katika mafunzo ya ujasiriamali na mbinu za ukuzaji wa biashara, yatakayotolewa na wakufunzi wa chuo hicho 


Akizungumza na blog hii mratibu wa mafunzo hayo Bwana Andrea Ngobole amesema kuwa: mafunzo hayo yatakuwa ya siku mbili kuanzia tarehe 19-20/09/2013na yanalenga kuwapa wanachuo hao juu ya mbinu na maarifa kuwa wajasiriamali na wafanyaiashara wenye mafanikio na kuwa chachu ya maendeleo kwa familia, jamii na taifa kwa ujumla

0 comments:

TAABU TUPU HUDUMA YA MAJI KITETO YAGEUKA KUWA BIASHARA


mji wa Kibaya wakiwa kwenye foleni ya maji ambapo imeelezwa ili kupata maji lazima kuwekwa foleni kwa siku tatu
Huduma ya maji Kiteto yageuka kuwa biashara

0 comments:

WAKUTWA CHOONI WAKILAWITIANA...BOSI AJITETEA ALIKUWA ANATAKA KUNYOLEWA NA MFANYAKAZI WAKE....!!



MDOSI au Kanjibai aliyefahamika kwa jina moja la Milah ambaye ni bosi wa kampuni moja ya ujenzi yenye makao yake Mwenge jijini Dar alinaswa chooni akiwa na mfanyakazi wake, John Carlos ‘Shabani’ (watu walimpachika jina la Shabani kutokana na Kanjibai wa kwenye Komedi) ikidaiwa walikuwa katika mazingira ya ulawiti, Ijumaa ‘Kubwa’ lina sinema yote.
Ishu hiyo nzito ilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo wawili hao walikuwa chooni humo kwa zaidi ya nusu saa na kuwasababishia usumbufu watu waliokuwa wakitaka kutumia choo hicho. 



KISA KILIPOANZA
Siku hiyo ya tukio, mtu mwenye sauti ya kiume alipiga simu kwenye chumba cha habari cha Global Publishers, Mwenge jijini Dar na kupasha juu ya tukio hilo. Alisema:
“Jamani hebu njooni haraka hapa kwenye hii kampuni ya ujenzi ya… (jina lipo) iko hapa Mwenge. Kuna bosi wetu mmoja amejifungia chooni na mfanyakazi mwenzetu kwa zaidi ya robo saa sasa, sijajua nini kinaendelea humo ndani. Sisi wengine hapa matumbo ya kuendesha yametushika sijui tufanyaje?!”
Mtoa habari huyo alikwenda mbele zaidi kwa kuwaambiwa mapaparazi wetu waliompokelea simu wachukue Bajaj au Bodaboda ili kuwahi.
Sosi huyo kabla ya kukata simu aliweka wazi ramani ya kufika kwenye choo hicho na kusisitiza kwamba muhimu kuwahi kwa sababu huenda wanagombana.

MAPAPARAZI WAWASHA PIKIPIKI
Kufuatia msisitizo huo, mapaparazi wetu makini  waliwasha pikipiki zao, kila mmoja na yake na kushika njia kuelekea eneo la tukio.
Hata hivyo, kwa kuamini wanaweza kukutana na lolote, waliona ni vyema kwanza kwenda kutoa taarifa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi cha Mwenge ambapo walipewa askari wawili kuelekea eneo la tukio.

ENEO LA TUKIO SASA
Timu hiyo iliwasili kwenye eneo la tukio. Mlango wa choo hicho ulikuwa umefungwa lakini kwa mara moja tu haikuwa rahisi kugundua kama ulifungwa kwa funguo au kawaida tu.
 Afande mmoja alijitolea kugonga mlango wa choo hicho ili kupima ushirikiano utakaotolewa na wawili hao au mmoja wao.
Sauti iliyoonekana ni ya Kanjibai kutokana na kushindwa unyoofu wa lugha ya Kiswahili ilisikika ikiuliza:
“Nani wewee… taka nini huku?”
Afande: Sisi ni askari polisi, fungua haraka tunajua mko wawili humo ndani, fungua.
Kanjibai: Subiri kidogo.
Baada ya dakika kadhaa ambazo mapaparazi wetu hawakuzifuatilia, mdosi huyo alifungua mlango na kukutwa akiwa na ‘Shabani’.

WALICHOKUWA WAKIKIFANYA CHOONI
Katika maswali ya harakaharaka nje ya choo hicho kila mmoja alisema la kwake ambalo aliliamini linaweza kumchomoa kwenye skendo hiyo mbaya.
‘Shabani’ alisema yeye aliingia kwenye choo hicho baada ya kuitwa na bosi wake huyo ambapo alishindwa kumkatalia kwa kuogopa kupoteza ajira yake na kama inavyojulikana maisha ya Dar bila kazi ni ngumu kuyamudu.
Alipoulizwa walichokuwa wakikifanya ndani ya choo hicho, Shabani alibaki akiwatumbulia macho maafande, wakati mwingine mapaparazi wetu.
Kwa upande wake Kanjibai alipotakiwa kujieleza kisa cha kuingia chooni na mfanyakazi wake, alisema alimuomba wazame humo ili akamnyoe. Yaani Kanjibai alitaka kunyolewa.

IKAFIKA ZAMU YA KUPELEKWA KITUONI
Afande mmoja aliamuru wawili hao wapelekwe kituo cha polisi, lakini kabla ya kuanza safari, mdosi huyo aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali na kutoa vitu vyake kadhaa na kuwakabidhi wadosi wenzake waliofika ‘kumsaidia’ muda mfupi baada ya kunaswa.
Halafu aliingiza mkono kwenye mfuko mwingine na kutoa mafuta aina ya KY  ambayo mtaani hujulikana sana kwa jina la ‘mlainisho’ lakini askari alimwambia mafuta hayo yanatakiwa kituoni kwa ajili ya ushahidi hivyo asiwape nduguze.
Breki ya kwanza ilikuwa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi Mwenge ambapo baada ya mahojiano mafupi walihamishiwa Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’ ambapo walihojiwa zaidi kuhusiana na tukio hilo.

 
Source: GP
L

0 comments:

AINA KUMI YA VYAKULA VINAVYOONGEZA UWEZO KATIKA TENDO LA NDOA



Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume na kuacha idadi ya wanawake wanaokabiliwa na tatizo hilo kwa mujibu wa uchunguzi kubaki na asilimia 13.

0 comments:

CHEKI WATOTO WACHANGA WANAVYOTUPWA! DU!!! INASIKITISHA SANA

Watoto wachanga baada ya kuzaliwa katika Manispaa ya Morogoro, ongezeko la wazazi kutupa watoto wao limekuwa likiongezeka nchini. Picha ya Maktaba.

0 comments:

Polisi mkoani Dodoma yashindwa kumfikisha mahakamani mbunge SUGU wa Mbeya mjini...!!



JESHI la Polisi mkoani Dodoma limeshindwa kumpandisha kizimbani Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kwa madai kuwa upelelezi bado haujakamilika.
Mbilinyi, maarufu kama ‘Sugu’ alifunguliwa jalada na jeshi hilo Ijumaa iliyopita, akidaiwa kumjeruhi jichoni askari wa Bunge, Koplo Nikwisa Nkisu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Wakili wake, Tundu Lissu, alisema kuwa hawakufikishwa mahakamani kama walivyotegemea kutokana na kuelezwa kuwa upelelzi haujakamilika.

Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kuwa baada ya mteja wake kuripoti kituoni aliambiwa kwamba upelelezi huo ukikamilika wataitwa ili kupewa maelezo ya hatua gani inafuata.

Alisema kitendo hicho cha polisi kuwaita bila kukamilisha upelelezi wao ni kuwapotezea muda.

“Nashangaa ni kwanini tunaitwa, tuliambiwa tufike hapa, lakini tulipokuja hapa hakuna jambo lolote la maana tuliloambiwa, badala yake wanasema tuendelee na shughuli zetu upelelezi haujakamilika na baada ya wiki mbili watatuambia kinachoendelea.

“Yaani, haya mambo yanayofanywa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi na Naibu wa Spika, Job Ndugai, ni ya ajabu sana. Tumeitwa kutoka mbali kote kwa ajili ya kuja hapa kuambiwa kuwa upelelzi haujakamilika,” alisema.

Aliongeza kuwa Sugu alitoka Mbeya huku naye akitoka huko alikokuwa kwa ajili ya kuja Dodoma lakini hakuna jambo lolote limefanyika, na kuhoji ni kwanini wasingearifiwa hata kwa simu.

Lissu alisema kuwa atashanga kama jeshi hilo litapeleka kesi hiyo mahakamani kwani kosa lenyewe lilifanyikia bungeni.
“Nitashangaa kama jambo hili litapelekwa mahakamani, kwani kwa mujibu wa kanuni, mbunge hatashitakiwa kwa jambo ambalo alilitenda akiwa katika maeneo ya Bunge.

“Mambo haya yalitokea tukiwa bungeni na huko kuna kinga ya mbunge. Mbunge akikosa anahukumiwa kwa mujibu wa kanuni, lakini kwa fikra na mashikinizo ya viongozi wa CCM wanataka kuvuruga na kufanya mambo kwa masilahi ya chama chao,” alisema.

Naye Sugu alisema kuwa kitendo kilichofanywa na Ndugai ni cha kihuni na wala hakikuwa na misingi yoyote hadi kulazimisha askari wa Bunge kumpiga.

0 comments:

SPIKA WA BUNGE NDUGAI AJIGAMBA KUMTOA FREEMAN MBOWE BUNGENISOMA HABARI HII HAPA


*Asema wanaompinga ni mbumbumbu wa kanuni za Bunge
NAIBU Spika, Job Ndugai ametetea uamuzi wake wa kuagiza kutolewa ndani ya ukumbi wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akisema alikuwa sahihi.

Mabishano hayo ambayo yalisababisha kuibuka kwa vurugu bungeni yalitokea mwishoni mwa wiki, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu, ambapo kiongozi huyo wa Bunge aliruhusu mjadala kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba uendelee.

Kutokana na hali hiyo, Mbowe alisimama kutaka kutoa ufafanuzi juu ya mjadala huo, lakini Ndugai alimzima na kumtaka kukaa chini, jambo ambalo halikumfurahisha Mbowe na kumfanya agomee agizo lake.

Akizungumza na MTANZANIA jana kwa njia ya simu, Ndugai alitumia muda mwingi kutetea uamuzi wake na kukosoa hoja za watu wanaompinga juu ya uamuzi wake huo.

Ndugai alisema katika kikao hicho, Mbowe alifanya jeuri kubishana na kiti na kueleza kuwa kanuni za Bunge zinasema hakuna mbunge yeyote atakayesimama kuzungumza bila kuruhusiwa na kwamba uamuzi wa kiti ndiyo wa mwisho.

Ndugai alisema wanaomtuhumu kwamba hakutenda haki kumuamuru Mbowe akae chini, wanafanya hivyo kwa vile hawajui kanuni za Bunge.

Ndugai alisema kwa mujibu wa kanuni, ni Rais wa Jamhuri pekee ndiye anayeruhusiwa kulihutubia Bunge kwa wakati anaoona yeye unafaa, lakini si mbunge.

“Hata rais mwenyewe ni lazima amwandikie barua spika, huu ndiyo utaratibu lakini si mbunge au waziri anayeruhusiwa kusimama kwa wakati anaoutaka yeye kuzungumza akaruhusiwa, ni lazima ataomba ruhusa kwa Spika na kama ipo nafasi ya kufanya hivyo Spika atamruhusu, kama haipo hataruhusiwa.

Alipoulizwa kwamba haoni kama alivunja kanuni kwa kumzuia Kiongozi wa Upinzani bungeni wakati kanuni za mabunge ya Jumuiya ya Madola zinatoa upendeleo kwa kiongozi huyo na waziri mkuu ndani ya Bunge, Ndugai alisema:

“Katika vikao vya Bunge, uamuzi wowote wa Spika unakuwa wa mwisho na hauwezi kupingwa na mbunge au waziri yeyote.

“Mbowe nilimuomba kwa heshima sana atupishe kwanza, nilimuelekeza karibu mara tatu…lakini mtu mzima anavunja utaratibu.

“Huyu Mbowe amejivunjia heshima mwenyewe, hata kanisani anayeendesha ibada ni mtu mmoja tu, na wengine wanapaswa kufuata utaratibu.

“Kwanza Mbowe alijitoa mwenyewe kwenye orodha kwa maandishi na ninayo hapa.... yeye na Halima Mdee, sasa alisimama kufanya nini kama sio ujeuri?

“Kanuni anazijua mimi ningemruhusu tu, lakini kwa ujeuri hakufanya hivyo. Kuna taratibu za bunge, mbunge anakaa chini pale Spika anaposimama na wasome kanuni, sasa hapo mjeuri ni nani?

“Tujifunze kanuni haiwezekani mtu yeyote asimame saa yoyote, kila mmoja hawezi kufanya anavyotaka, kuna taratibu zake, kiti kikimuona atapewa nafasi kama ipo na iwapo kiti kikiridhika,” alisema Naibu Spika.
                                                    source bossngasa

0 comments:

MWANAMKE ALIYEBADILI JINSIA NA KUWA MWANAUME AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME...



Mwanaume mmoja aliyebadili jinsia ni wa kwanza barani Ulaya kujifungua mtoto baada ya kuwa mjamzito kwa njia ya kupandikiziwa mbegu za kiume.
Mwanaume huyo ambaye hakutajwa jina, ambaye alizaliwa mwanamke, alijifungua mtoto wa kiume nyumbani kwa msaada wa mkunga katika wilaya masikini ya Neukoellin ya mjini Berlin.

Alisisitiza kujifungulia nyumbani sababu alikataa kuorodheshwa kama mama kwenye nyaraka zozote za hospitali - hitaji la kisheria nchini Ujerumani.
Baba huyo, ambaye alibakisha viungo vya uzazi vya mwanamke, amekuwa akifanyiwa tiba za kubadilishwa homoni kwa miaka kadhaa kubadili jinsia.

Habari zaidi kuhusu upandikizwaji mbegu au taarifa za uhusiano wowote zimehifadhiwa kutolewa hadharani kutokana na baba huyo kutaka kumlinda mtoto wake huyo.

Rasmi mtoto huyo, ambaye alizaliwa Machi 18, hana mama, ana baba pekee.

Msemaji wa Mambo na Ndani wa Berlin alisema: "Mtu huyo aliyezusha maswali hakutaka kujitokeza kama mama ila baba kwenye cheti cha kuzaliwa na matakwa hayo yameheshimiwa."

Baba huyo mtarajiwa pia alitaka kwamba jinsia ya mtoto huyo 'isifichuliwe kwa namna yoyote'. Lakini mamlaka zilipuuza hilo na kutangaza kuwa ni wa kiume.

Vyombo vya habari vya Ujerumani viliibuka kwa namna ya kushangaza katika habari ya uzazi huo wa kubadili jinsia.

'Baby belly instead of a beer belly!' (Kitambi mtoto badala ya kitambi bia!") kilikuwa moja ya vichwa vingi vya habari kwenye magazeti ya Ujerumani yakiripoti kuzaliwa kwa mtoto huyo.

Wakati huohuo, Falko Liecke, diwani wa wilaya hiyo ambako mtoto huyo alizaliwa, alisema: "Hiki ni kitu ambacho sikuwahi kusikia maishani ana kushuhudia."

Mwaka 2011 Mahakama Kuu ya Ujerumani iliamuru kwamba mtu binafsi hatakiwi kuondolewa viungo vyake vya uzazi awe mwanamke au mwanaume 'kupata kutambuliwa hadharani kisheria kwa jinsia atakayowekewa'.

Ndio maana baba huyo wa mtoto wa hivi karibuni amekuwa mwanaume wakati akiendelea kuwa na viungo vyake vya uzazi vya kike.

Dk Tobias Pottek wa Hospitali ya Asklepios West mjini Hamburg alisema: "Hata kama mwanamke anataka kuishi kama mwanaume na kuwekewa homoni kuotesha ndevu, kwa kuwa mji wa mimba na mayai bado yapo, pia inawezekana kupata ujauzito.

Hili ni jambo la kwanza la mtoto kuzaliwa barani Ulaya wa mzazi aliyebadili jinsia, lakini katika Marekani jambo la Thomas Beatie, mwanaume aliyebadili jinsia ambaye alikuwa na watoto watatu, linafahamika mno.

Beatie alikuwa akidai talaka kutoka kwa mkewe, lakini alikataliwa sababu jaji hakuweza kuthibitisha kama alikuwa mwanaume wakati akifunga ndoa.

Jaji huyo aliamua hakukuwa na mamlaka ya kisheria ya kuomba talaka kama ndoa hiyo haikuwa ikitambuliwa.

0 comments:

TAZAMA PICHA 29 ZA WAREMBO MISS TANZANIA 2013:

 
CLARA BAYO.

0 comments:

BEHIND THE SCENES.RAY AND JACKLINE WOLPER STARS IN A NEW MOVIE,

Vicent Kigosi(Ray) and Swahili movies' sexy diva Jackline Wolper will be seen in a new flick. The two megastars in Swahiliwood have already shared screen space together in some movies including Surprise and currently they are shooting their new project by Rj Company. Look behind the scenes of the movie..............

  Ray and Wolper on set



0 comments:

MWANAMKE ANASWA NA SARE ZA JWTZ


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemkamata Saida Mohamed (30), mkazi wa Mwasonga Kigamboni, akiwa na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

0 comments:

MASANJA MKANDAMIZAJI AMWAGA MACHOZI BAADA YA KUSINGIZIWA KUWA ANAUZA BANGI


 Jana zilisambaa  habari  kwamba  masanja  mkandamizaji  na  msanii Diamond  wamedakwa  na  polisi  na  possport  zao  za  kusafiria  zimezuiwa....

0 comments:

TAZAMA PICHA NA VIDEO YALIYOJIRI KWAENYE UZINDUZI WA VIDEO YA JUX IKIAMBATAN NA BARTDAY YAKE:

DSC_0062

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz