FFU WAPINDUKA NA GARI LAO NA MMOJA WAO KUFARIKI PAPO HAPO

ASKARI mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoani Kilimanjaro, Fidelis Mwaliyatabu, amefariki dunia papo hapo na wengine tisa akiwamo Mkuu wa Kikosi hicho kujeruhiwa vibaya baada ya gari lao kupinduka katika kijiji cha Kilingi, wilaya ya Siha, wakati wakienda kuzima vurugu za wananchi.
Ajali hiyo ilitokea wakati kikosi hicho kikielekea katika kijiji cha Karansi kwa ajili ya kukabiliana na wananchi waliokuwa wakiandamana kupinga wenzao waliokamatwa usiku wa manane baada ya kuvamia mashamba mali ya Shirika la Roho Mtakatifu-Kilasara.
Taarifa kutoka kijijini humo zilieleza kwamba wanakijiji waliamua kuandamana baada ya wenzao watano kukamatwa na Jeshi la Polisi nyakati za usiku kwa mahojiano kutokana na kukabiliwa na tuhuma za kushawishi wanakijiji wenzao kuvamia maeneo ya Shule ya Kilasara na kusababisha hasara kubwa kwa shule hiyo.
Kufuatia kukamatwa kwa watuhumiwa hao, wanakijiji waliamua kuaandamana hadi katika kituo cha polisi ili kuwatoa wenzao hali ilisababisha jeshi hilo kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya, jambo ambalo lilishindikana kutokana na wingi wa watu walikuwa wanaandamana.
Inadaiwa kuwa wananchi hao walijikusanya na walianza kuandamana kuanzia majira ya saa 7 usiku kuelekea kituo cha polisi ili kuwatoa wenzao walikuwa wanashikiliwa.
Wananchi wanaoshikiliwa na jeshi hilo ni John Sokoine, Abeli Solomoni, Christopher Solomon na aliyetambuliwa kwa jina moja tu la Julius. Wote walikamatwa usiku wa kuamkia jana.
Mnamo Juni 11, mwaka huu majira ya mchana wananchi wa kijiji hicho walivamia eneo lenye ukubwa wa hekta mbili na kufyeka mazao mbalimbali yaliyokuwa shambani hapo kwa madai kuwa wamiliki wa shule hiyo wamechukua eneo hilo kinyume cha taratibu.
Kwa upande wake, Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, Kanda ya Afrika, Padri Jerome Okama, aliushutumu uongozi wa kijiji hicho kwa kuvifumbia macho vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi wakati wakitambua kuwa eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 8.9 linamilikiwa na shirika hilo kihalali.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Robert Boaz, akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu kutoka wilayani humo jana jioni, alisema askari hao walipata ajali hiyo majira ya saa 6.45 mchana katika kijiji cha Kilingi nje kidogo ya mji wa Sanya Juu.
Alisema askari hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC na wengine wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu ya Kibong'oto ilioyopo wilayani Siha na kwamba watano kati yao hali zao ni mbaya.
Alitaja gari la Polisi lililopinduka na kuua kuwa ni Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2070 lililokuwa likiendeshwa na Sajenti Herman Dancan. Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi na kuacha njia na kupinduka.
Aliwataja waliojeruhiwa katika ajali hiyo kuwa ni Mkuu wa FFU mkoani hapa, ASP Nonino, Renatus Misigalo, Alfonce Joseph, Koplo Elifuraha Lenare, Peter Albert, Bashiri Yusuph, George Mwakyusa na Gaspar Mwapunda.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Kibong'oto

0 comments:

"WANAOPINGA KODI YA LINE ZA SIMU NI WANAFIKI WASIOPENDA MAENDELEO "....MIZENGO PINDA


WAKATI Serikali ikiahidi kutazama upya tozo ya Sh 1,000 kwa laini za simu ili kupunguza mzigo kwa wananchi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema tozo hiyo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini.CONTINUE READING

Alisema hayo alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Songea juzi, katika ziara yake ya wiki moja mkoani Ruvuma, baada ya kuutembelea mkoa mpya wa Njombe.


“Ni kama vile tozo iliyoongezwa kwenye mafuta ya petroli, ambayo imetupa fedha nyingi kwenye Mfuko wa Barabara, za kuunganisha miji na mikoa na nyingi zimejengwa na zinaendelea kujengwa.



“Nani asiyetaka vijiji vipate umeme kama miji, ili usaidie kuondoa giza, uendeshe viwanda vidogo vidogo na usaidie kukuza uchumi? Wanaopinga tozo hii, hawatutakii mema,” alisema Pinda.


Bunge la bajeti lililomalizika mwezi uliopita, lilipitisha tozo ya Sh 1,000 kwa matumizi ya simu za mikononi, ili fedha zitakazopatikana zisaidie katika mpango mkubwa wa kueneza umeme vijijini unaoendeshwa na Wakala wa Umeme Vijijini, (REA). Kwa mkoa wa Ruvuma peke yake, vijiji vipatavyo 150 vitapatiwa umeme chini ya mpango huo.


Katika mikoa yote nchini kuna idadi inayotofautiana ya vijiji vingi vitakavyonufaika katika mpango huo. Umeme umo katika sekta ya nishati ambayo ni moja ya sekta sita zilizoteuliwa kutekelezwa chini ya mpango wa kuhakikisha matokeo makubwa yanapatikana sasa, wenye upeo wa miaka mitatu, kuanzia mwaka huu wa fedha wa 2013/14. Sekta nyingine ni Kilimo, Uchukuzi, Maji, Elimu na Mapato.


Kabla ya mkutano wa hadhara, Waziri Mkuu alizindua Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi cha Songea, kinachodahili zaidi ya wanafunzi 500 na kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa mfundi stadi mbalimbali.



Awali Waziri Mkuu Pinda alisema bei ya mahindi kutoka kwa mkulima katika mkoa wa Ruvuma, itakuwa ni Sh 500 kwa kilo badala ya Sh 450, ili wakulima wahamasike kuuza mahindi kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).


Mkoa wa Ruvuma ni moja ya mikoa inayozalisha mahindi, chakula kikuu nchini kwa wingi na NFRA inatarajia kununua tani 50,000 kutoka katika mkoa huo.


NRFA imepangiwa kununua zaidi ya tani 200,000 nchini kote kwa ajili ya hifadhi ya chakula, kiwango kikubwa kuliko mwaka uliopita.


Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Pinda pia aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa soko la kimataifa katika kijiji cha Mkenda kwenye mpaka na Msumbiji, ikiwa ni moja ya masoko 48 yatakayojengwa mipakani kurahisisha biashara na kukabiliana na magendo. Leo Waziri Mkuu ataondoka Songea kurejea Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara yake mkoani humo

0 comments:

HUYU NDO MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTRE ALIYEMWAGIWA TINDIKALI




MSHTUKO mkubwa ulijiri Jumamosi iliyopita, ikiwa ni baada ya kusambaa kwa habari za kumwagiwa tindikali, mfanyabiashara mwenye ‘levo’ ya ubilionea, Said Said Mohammed, 42, ambaye ndiye mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Home Shopping Centre    
 Said ambaye kwa utambulisho mwingine anajulikana kama Said Mohammed Saad, alimwagiwa tindikali Ijumaa iliyopita, saa 2 usiku, lakini habari zake zikavuma Jumamosi, hivyo kuibua taharuki ya aina yake.

Kuhusu nani alimmwagia tindikali hiyo, sababu ya kutendwa unyama huo, yupi mhusika mkuu wa ukatili wenyewe na malengo ya uharamia, kwa jumla, hayo ni maswali yanayoendelea kuitesa familia yake, watu wa karibu pamoja na Jeshi la Polisi Tanzania.


Taarifa za kipolisi zinathibitisha kwamba alimwagiwa tindikali akiwa anazungumza na mfanyakazi wake wa duka lake lililopo kwenye Jengo la Msasani City Mall kisha akakimbizwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, iliyopo Masaki, Dar es Salaam kabla ya kupelekwa Afrika Kusini kwa ndege ya kukodi ndani ya kipindi kisichozidi dakika 60.

SAID NI NANI?
Ni Mtanzania mwenye asili ya Bara la Asia. Inadaiwa kwamba ndugu zake wengi wana asili ya nchi za Yemen na Saudi Arabia.



Ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Center. Kampuni hiyo ina maduka mengi Dar es Salaam na katika mikoa kadhaa ambayo yanahusika zaidi na uuzaji wa vitu vya nyumbani na ofisini.


Anatajwa kuwa tajiri mwenye uwezo zaidi katika jumuiya ya wafanyabiashara wa eneo la Kariakoo, kifedha na ushawishi.
Inadaiwa kwamba wafanyabiashara wengi wenye maduka yao Kariakoo, humtegemea yeye kuingiza mizigo nchini, kutokea nje ya nchi hususan China.


Anamiliki nyumba kadhaa za ghorofa Kariakoo, yapo madai kwamba anamiliki nyumba sita.


Baadhi ya majengo ambayo anahusishwa nayo, la kwanza lina ghorofa saba, lipo Mitaa ya Swahili na Msimbazi, la pili lina ghorofa sita, lipo Kongo na Aggrey, tatu ni la ghorofa nne, lipo Barabara ya Uhuru na kadhalika.

Said kupitia kampuni yake ya Home Shopping Centre, aligeuka nyota ya jaha kwa familia 655, zilizokumbwa na mafuriko eneo la Jangwani, Desemba 2011 kisha kuhamishia Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam.


Kwa moyo wake mwema, Said aliidhinisha kila familia ipewe seti kamili ya vyombo vya nyumbani pamoja na taa zinazowaka kwa kutumia nishati ya mwanga wa jua.


Misaada hiyo, ilikabidhiwa na mkurugenzi mwingine wa Home Shopping Centre, Ghalib Said Mohammed ambaye ni mdogo wa Said. Misaada hiyo, ilipokelewa na Rais Jakaya Kikwete, Januari mwaka jana.

Said hakuishia hapo, baada ya misaada ya vyombo na taa za nishati ya mwanga wa jua, alifanya jambo jema zaidi kwa kujenga shule ya msingi, madarasa yote pamoja na ofisi za walimu, vilivyojengwa kwa ufadhili wa Home Shopping Centre.
 

Machi mwaka huu, shule hiyo ilizinduliwa na Rais Kikwete ambaye alikiri kwamba ujenzi wake utarahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwenye eneo hilo.



Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam, Yusuf Mrefu, alisema kuwa uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio la Said kumwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu.
 


Mrefu alisema, Said alikuwa akizungumza na mfanyakazi wake nje ya duka lake kwenye Jengo la Msasani Mall kisha akatokea kijana mrefu mwembamba ambaye alimmwagia kimiminika kinachosadikiwa kuwa ni tindikali.
 


Kamanda huyo wa polisi aliongeza kwamba mfanyakazi huyo wa Said, Hassan Ahmad, naye alijeruhiwa kidogo katika purukushani hiyo lakini alipopelekwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, alitibiwa na kuruhusiwa.

Iadaiwa kuwa Hassan, alipata majeraha baada ya kuanguka, wakati akimfukuza jamaa huyo ambaye alimmwagia tindikali Said.

Mmoja wa wauguzi katika Hospitali ya Ami Wellness, alimwambia mwandishi wetu kwamba baada ya Said kufikishwa pale, ilichukua kama nusu saa, akachukuliwa kupelekwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, tayari kwa safari ya kwenda Afrika Kusini.
 


“Hali yake ilikuwa mbaya, lile jicho moja limeathirika sana, kwa kweli sijui kama litaweza kuona tena. Ila moja litakuwa salama, ukizingatia amepelekwa katika hospitali yenye ubora zaidi. Yule mfanyakazi wake aliumia kidogo tu, alitibiwa na kuruhusiwa siku ileile,” alisema muuguzi huyo.
 

Kuhusu jina la hospitali aliyopelekwa, alisema: “Hakukuwa na utaratibu wa kuandika rufaa, alichukuliwa tu kupelekwa Afrika Kusini na sasa naamini anaendelea na matibabu vizuri. Ila inasikitisha sana, naamini wahusika walitaka kumfanya awe kipofu.”

Kwa mujibu wa taswira ya tukio lenyewe, kitendo alichofanyiwa ni umafia na mambo kadhaa yanafaa kumulikwa kwa undani. Mambo hayo ni;
Said ana uadui na nani? Aliyemmwagia alijuaje kama yupo pale? Kwa nini tindikali machoni?
 

Ni wazi Said anao maadui ndiyo maana kitu kile kimetendeka. Bila shaka aliyemmwagia aliambiwa na mtu, huyo anafaa kupatikana. Bila kupindisha ukweli ni kwamba mmwagaji alikusudia kumfanya Said awe kipofu.
 

Polisi wanatakiwa kuchunguza nyendo za Said, kuona ana uhasama na akina nani katika biashara au hata kwenye mambo ya kijamii. Kadhalika, ichunguze mawasiliano ya watu wa karibu na Said, atajulikana mtoa taarifa, hivyo kumpata mhusika wa ukatili pamoja sababu ya unyama wenyewe.

SKENDO ZA SAID
Said ameshawahi kuripotiwa na vyombo vya habari katika kashfa mbalimbali, gazeti moja liliwahi kuandika matoleo kadhaa, likimtaja kama mfanyabiashara hatari kwa nchi ya Tanzania.
 

Vilevile, alishawahi kuripotiwa kumfanyia unyama, kijana mmoja raia wa Lebanon ambaye alidaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na dada yake.

0 comments:

BOMU JINGINE LALIPUKA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA.....POLISI WAKIRI KUHUSIKA NA MLIPUKO HUO..!!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidNZcZ-D2Rj8guDTQEYrfgFERkHVadyhuK-_3YDl7i9ZEfIbTyEcKKG_Pn6gPR9R6OJmn9TilO8Op2PgKuMR7QY6HTLbm_u412pYR4Iy9i51WalfrWHzRbQ080iotzDTDdED5ZS1KfbeUK/s640/2+%287%29.JPG

Ikiwa ni takribani mwezi mmoja tu tangu bomu lilipolipuka kwenye mkutano wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mkoani Arusha, jana tukio kama hilo lilitokea jijini Dar es Salaam kwenye mkutano wa Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, ambao aliutishia kwa lengo la kuwaelezea wananchi mrejesho wa yaliyojiri bungeni hivi karibuni na kuhamasisha wananchi kushiriki kutoa maoni kwenye rasimu ya Katiba mpya.

Tofauti na Arusha, jana bomu hilo lililipuka likiwa kwenye gari la Polisi waliokuwa kwenye mkutano huo katika viwanja vya Sahara, katika Kata ya Mabibo jijini Dar es Salaam na kuibua taharuki kubwa kwa wananchi na wafuasi wa Chadema waliokuwa wamehudhuria mkutano huo.

Polisi wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kwamba bomu hilo lililipuka kwa bahati mbaya na kwamba ni la jeshi hilo.


Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kinondoni, Yusuf Mrefu, alisema mlipuko huo ulitokea kwa bahati mbaya na kwamba haikuwa nia ya polisi kutumia nguvu au kuzuia mkutano wa Chadema.

 "Ni bomu la mkononi. Polisi walikuwa na mazungumzo na viongozi wa Chadema na siyo kwamba kulikuwa na vurugu au matumizi ya nguvu, ni tukio la bahati mbaya," alisema.

Mrefu alisema pia kwamba Polisi haikuwa imepanga kupiga mabomu kwenye mkutano huo wala kuuzuia.

"Siwezi kueleza limetengenezwa wapi, ni aina gani au kazi yake; kwa sababu mimi mwenyewe nimepewa taarifa kwa simu, sikuwa eneo la tukio, nilikuwa kwenye msafara wa Makamu wa Rais,"
alisema.

Aidha, Kaimu Kamanda huyo bila kufafanua alisema: "Halina madhara." Hata hivyo, alipoulizwa kazi ya bomu hilo ikiwa halina madhara, alijibu kwamba asingeweza kueleza zaidi kwa kuwa hakuwa na taarifa za kina kwa kuwa hakuwa eneo la tukio.

Hata alipoulizwa jina la kitaalamu la bomu hilo alisema hana taarifa za kina.

Wakati Polisi wakieleza hayo, mashuhuda pamoja na taarifa zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zilidai kwamba mtu mmoja alijeruhiwa kwenye tukio hilo.

Taarifa zinaeleza kwamba mlipuko huo ulitokea baada ya Mnyika kwenda kwenye gari ya Polisi kwa nia ya kuwasalimia na ndipo kishindo kilichoashiria mlipuko wa bomu kilisikika.

Kufuatia tukio hilo, mkutano huo ulipigwa marufuku na kuhamishiwa eneo la Ubungo Mataa ambako ulifanyika.

 Diwani wa Ubungo (Chadema), Boniface Jacob, akifungua mkutano huo alisema waliamua kuchukua vibali viwili vya mkutano huo kwa tahadhari cha Mabibo na cha Ubungo.

Akizungumzia kuhusu tukio hilo wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Ubungo jana, Mnyika alidai kuwa waliomba kibali cha kufanya mkutano huo siku tano kabla kwa kuwaandikia polisi barua, lakini hawakuwajibu hadi jana asubuhi wakiwataka kusitisha kwa sababu kulikuwa na ziara ya Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, kukagua shughuli za usafi jijini Dar es Salaam.

Mnyika alisema aliwajibu polisi kuwa hawezi kupokea taarifa za kusitisha mkutano wake huyo kwa simu bali aliwataka wampe kwa maandishi.

Alisema baadaye polisi waliandika barua ya kumuagiza asitishe mkutano wake huo kupisha ziara ya Makamu wa Rais.

Alisema hata hivyo, alipoangalia ratiba ya ziara ya Makamu wa Rais, aligundua kuwa haikugusa jimboni mwake na kuwaomba tena polisi wamruhusu kufanya mkutano huo.

Alisema alimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova na kujibiwa yuko nje ya nchi, hivyo aliwaomba wasaidizi wake wampe kibali lakini hawamkujibu na kumuomba asubiri wajadiliane kwanza.

Mnyika alisema kutokana na muda kuyoyoma, alimtafuta Mkuu wa Jesh la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Said Mwema, kumuomba amsaidie, lakini aligonga mwamba baada ya kumjibu kuwa hawezi kutengua maamuzi yaliyotolewa na kiongozi wake wa chini na kumtaka aandike barua nyingine ya kuomba kibali cha kufanya mkutano.

"Wakati naendelea kuwasiliana na viongozi wa polisi kuomba wanipe kibali, nilikuwa tayari kwenye viwanja vya Sahara na ndipo zikaja defender (magari ya polisi) tatu za polisi," alisema na kuongeza kuwa:

"Ziliposimama niliwafuata na kwenda kuwaambia kuwa vipi tena mbona mmekuja wakati nimeomba kibali cha kufanya mkutano, ndipo lilipolipuka bomu hilo ndani ya gari ambalo nami nilikuwa nimesimama karibu nalo."

Alisema baada ya kulipuka bomu hilo, watu walikuwa wamekusanyika katika viwanja hivyo walikumbwa na taharuki na kukimbia ovyo kunusuru ya maisha yao. Kwa mujibu wa Mnyika, wakati watu hao wakikimbia ovyo, alikwenda lilikoangukia bomu hilo kumuwahi majeruhi, Thomas Jarome.

Alisema polisi nao walikwenda kumuwahi majeruhi huyo na kumbeba 'mzobemzobe' wakati wakitaka kumuingiza kwenda gari lao, Mnyika na viongozi wengine wa Chadema waliwazuia na kumpeleka hospitalini ambako alipatiwa matibabu na kuruhusiwa kuondoka.

Alisema wakati majeruhi huyo akiendelea kupatiwa matibabu, viongozi wa chama hicho walikusanyika na kujadili sehemu nyingine ya kwenda kufanyia mkutano wao na kubaini kuwa Diwani wao wa Ubungo alikuwa na kibali cha kufanya mkutano eneo la Abiani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Aliwatangazia wananchi wafuasi na wapenzi wa Chadema wakiwaomba wahamie Abiani.

Katibu wa Mbunge wa Ubungo, Gastone Garubindi, alidai bomu hilo lilipigwa na polisi kwa lengo la kuwatisha wananchi wasihudhurie mkutano huo.

Akizungumza na NIPASHE majeruhi Jerome, alidai kuwa polisi walikusudia kulipua bomu hilo kwani lilikuwa mikononi mwao na askari waliopata mafunzo ya kutosha kuhusu milipuko.

Alisema baada ya kujeruhiwa, viongozi wa Chadema walimpeleka katika kituo Mabibo ambako alipewa PF3 na kwenda zahanati Tandale na kutibiwa.

Jerome alisema baada ya kutibiwa aliruhusiwa kurejea nyumbani na kutakiwa kurudi leo kwa uchunguzi zaidi na kuchomwa sindano ya pepopunda (tetanus).

Tukio la jana limekuja huku uchunguzi wa mlipuko wa bomu uliotokea Juni 15, mwaka huu katika viwanja vya Soweto, Kata ya Kaloleni mkoani Arusha kwenye mkutano wa kufunga kampeni za udiwani wa Chadema, ukiwa bado unaendelea. Katika tukio hilo, watu watatu walipoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya. Bomu hilo linaelezwa kuwa lilipuka kwenye mkusanyiko wa watu mita chache kutoka jukwa kuu, wakati mkutano huo ulipokuwa umekwisha na shughuli ya kukusanya michango ikiendelea.

Viongozi wa juu wa Chadema, Freeman Mbowe na Godbless Lema walikuwapo kwenye eneo hilo.

Hadi sasa hakuna mtu ambaye amekamatwa kuhusiana na mlipuko huo pamoja na kwamba Serikali imetangaza donge nono la Sh. milioni 100 kwa mtu atakayefanikisha kukamatwa kwa mhusika au wahusika wa tukio hilo.

Zaidi ya watu 70 walijeruhiwa baada ya tukio hilo kufuatia polisi kufyatua risasi za moto kwa nia ya kukabiliana na wananchi waliokuwa wanawashambulia.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alikaririwa akieleza kwamba bomu lililolipuka Arusha lilitengenezwa China.

Aidha, Septemba, 2012 aliyekuwa Mwakilishi wa Kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa, Daudi Mwangosi, aliuawa kwa kupigwa bomu la machozi na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) eneo la Nyololo Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

Alipigwa bomu hilo baada ya kupokea kipigo kutoka kwa baadhi ya askari wa FFU waliokuwa wakiizuia Chadema kuendesha harakati zake za kufungua tawi la chama hicho katika eneo hilo.

Mwangosi ambaye pia alikuwa  Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), aliuawa mbele ya wananchi, askari wa FFU na aliyekuwa  Kamanda wa jeshi hilo mkoani humo, Michael Kamuhanda.

Askari huyo anayedaiwa kumuua Mwangosi, Pacificus Cleophase Simon (23), alikamatwa na kufikishwa mahakamani akikabiliwa na tuhuma za mauaji hayo na kesi hiyo bado inaendelea kutajwa

0 comments:

ASKARI WA JWTZ WALIOUAWA DARFUR KUAGWA LEO MAKAO MAKUU YA JESHI



Askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa katika jimbo la Darfur nchini Sudan, wanatarajiwa kuagwa leo kwenye viwanja vya makao makuu ya jeshi hilo.

Miili ya wanajeshi hao iliwasili nchini juzi kwa ndege maalumu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J. K Nyerere, Terminal One na kwenda kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Lugalo jijini Dar es Salaam.


Wanajeshi waliouawa ni Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Rodney Ndunguru, Peter Werema na Fortunatus Msofe.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya JWTZ, ilieleza kuwa askari hao wataagwa leo na shughuli hiyo itahudhuriwa na familia, makamanda wa jeshi na viongozi wa Serikali.
 

“Shughuli ya kuaga kwa heshima za kijeshi itaanza saa tatu kamili asubuhi katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga na itaendelea mpaka mchana kabla ya kusafirishwa,” ilisema taarifa hiyo.
 

Wanajeshi hao ambao ni miongoni mwa askari wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha Kulinda Amani katika Jimbo la Darfur nchini Sudan, waliuawa kutokana na mashambulizi ya kushtukiza yaliyofanywa na waasi wanaopigana na Serikali, hivyo kuwa ni mara ya kwanza kwa idadi kubwa ya wanajeshi wa Tanzania wanaolinda amani katika nchi mbalimbali kuuawa kwa wakati mmoja

0 comments:

WATOTO WAWILI WABAKWA NA BABA ZAO JIJINI DAR



Ukatili wa kutisha umewakuta watoto wawili wa familia tofauti wakidaiwa kubakwa na wazazi wao huku mmoja akifanyiwa unyama huo na baba yake mzazi na mwingine baba yake mdogo.

Habari zilizopatikana kutoka kwa ndugu, wazazi na majirani wa watoto hao zilisema kuwa wote walifanyiwa ukatili huo siku moja kwa nyakati na mazingira tofauti wilayani Temeke, Dar hivi karibuni.

Watoto hao ambao wote walifikishwa siku moja katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke kwa matibabu, walieleza jinsi walivyotendewa unyama huo wa kusikitisha ambao mzazi au mlezi hapaswi kumtendea mwanaye.

Wakwanza ni Anifa (8) ambaye alieleza kuwa alibakwa na baba yake mdogo aliyemtaja kwa jina moja la Amani.
Wapili ni Prisca ambaye alimweleza mwanahabari wetu kuwa alibakwa na baba yake mzazi aliyemtaja kwa jina moja la Charles.


Wakizungumza na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti wakiwa wodini hospitalini hapo wakiuguzwa majeraha, watoto hao waliokuwa sambamba na mama zao, walieleza kwa kina kile walichofanyiwa na wazazi wao.

Anifa alisema mara nyingi baba yake mdogo alikuwa akimpa pipi na akimuonesha muvi za picha za utupu na kumshawishi wafanye uchafu huo.


“Kuna wakati alikuwa akiniambia atanipa pesa lakini pia alinitisha kwa kisu au panga ili nimpe, nikawa nakataa lakini siku hiyo usiku alinibaka huku amenishikia kisu,” alisema mtoto Anifa kwa huzuni.

Kwa upande wake, Prisca alisema baba yake alimwambia atampa pesa ili wafanye mapenzi na wakati anamwingilia alikuwa ameshika noti ambayo hata hivyo alishindwa kusema ilikuwa na thamani gani.

Moja kati ya mambo yaliyoibua maswali ni kama kweli wabakaji wa watoto hao ni baba zao?


Ili kupata majibu  mwandishi wetu alizungumza na watoto hao kwa kina juu ya ukweli kama wahusika wanawafahamu vizuri ambapo katika mahojiano hayo yaliyorekodiwa, kila mmoja alikiri kuwa wanawajua fika wazazi wao hao.

Bila kupepesa macho wala kuogopa, mtoto Anifa alikiri kuwa mbakaji wake ni baba yake mdogo ambaye mara nyingi alikuwa akimtishia ili afanye naye mapenzi bila mafanikio hadi siku aliyopata nafasi usiku.

Kilichowashangaza wengi ni umri mdogo wa watoto hao kwani mtoto Anifa ana miaka nane huku mwenzake akiwa na umri wa miaka mitano.
 

“Mwanangu ana miaka mitano tu, sasa najiuliza huyu baba yake alikuwa anatafuta nini kwake, kwa kweli imeniuma sana na nimechanganyikiwa kwa kitendo alichofanyiwa na baba yake,” alisema mama wa Prisca huku mama wa Anifa akithibitisha umri wa mtoto wake kuwa ni miaka minane akiwa ni denti wa darasa la tatu katika shule ya msingi (jina kapuni).

Mama mzazi wa Prisca aliyejitambulisha kwa jina moja la Maria, alisema alishitushwa na taarifa za mumewe kumbaka mtoto wao.
 

“Nimeshaachana na mume wangu na sasa ameoa mwanamke mwingine, kwa kweli niliumia sana baada ya kupata habari za mwanangu kubakwa na baba yake.
 

“Nilikwenda Polisi Chang’ombe (Dar) nikamfungulia jalada la kesi namba CHA/RB/6028/2013-UBAKAJI ambapo mtuhumiwa alikamatwa na sasa yupo mahabusu katika Gereza la Keko akisubiri kesi yake kusikilizwa,” alisema mzazi huyo.
 

Kwa upande wa Anifa, shangazi yake aitwaye Wamoja alisema kuwa mtuhumiwa wa ubakaji wa Anifa alikamatwa mara alipokwenda hospitalini hapo kwa ajili ya kumjulia hali mgonjwa.
 

“Alijifanya hajui chochote akaja hospitali kwa kuwa Anifa alishamtaja kule polisi, ndipo akakamatwa na kufikishwa polisi Chang’ombe akisubiri kufikishwa mahakamani,” alisema Wamoja.
Baadhi ya mashuhuda wa matukio hayo, walishangazwa na madai ya watoto hao kubakwa na wazazi wao ambapo walisema kuwa siyo bure, lazima kuna kitu nyuma ya pazia

0 comments:

MASIKINI YA MUNGU YATIMA AMWAGIWA MAJI YA MOTO NA BINAMU YAKE


 Alivyounguzwa mgongoni
 Mtoto Dora Juma (12) akiwa na majeraha mwilini
Dora akiwa na msamaria mwema aitwaye Kauthari Issack


Mtoto Dora Juma,12, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Wazo Hill, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam imedaiwa ameunguzwa kwa maji ya moto na binamu yake aliyetajwa kwa jina la Saum Masud.

Dora ambaye ni yatima alikutwa na dhahama hiyo hivi karibuni eneo la Wazo Dar alikokuwa akiishi na binamu yake huyo kama mlezi wake baada ya kufiwa na baba yake.

Akisimulia tukio hilo Dora alidai kuwa siku ya tukio aliamka asubuhi kufanya usafi wa uwanja nyumbani na akaingia katika banda la bata kwa ajili ya kulisafisha.

“Baada ya kumaliza usafi niliingia ndani na kukuta kiporo cha ugali nikakata kipande nikawapa bata bandani, wakati huo dada (Saum) alikuwa amelala, alipoamka na kukuta kiporo cha ugali kimekatwa aliniuliza nikamueleza nimewapa bata, hakuamini.

“Akaniambia twende bandani kuangalia kama nasema kweli, tulifika tukakuta bata wameula hali iliyomfanya dada kutoamini, alinifunga mikono na miguu na kuniunguza kwa maji ya moto sehemu mbalimbali mwilini,” alidai Dora.

Alisema baada ya kufanyiwa unyama huo hakupewa huduma yoyote na kusababisha vidonda kuoza na aliokolewa na ndugu yao mmoja aliyekwenda kuwatembelea na kutaka kumnyoa nywele.

“Aliniambia nivue fulana ili nywele zisinidondokee, nilipovua alishangaa kuona nina vidonda mwilini, nilipomueleza mkasa mzima aliwapigia simu ndugu wengine hali iliyofanya dada Saumu kukimbia na kwenda kusikojulikana,” alidai.

Dora alisema alichukuliwa na msamaria mwema aitwaye Kauthari Issack ambaye alisema kuwa  kweli alimchukua binti huyo baada ya kuguswa na unyama aliofanyiwa.

“Baada ya kumchukua nilikwenda polisi kupata PF3 ili akatibiwe na anaendelea kutibiwa, askari wakafungua jalada namba KW/RB/6034/2013 na wakaanza kumsaka mtuhumiwa lakini wakafanikiwa kumkamata mumewe aitwaye Hamisi Kayanda ili aisaidie polisi,” alisema Kauthari.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni ACP Camillius Wambura amethibitisha mtoto huyo kufanyiwa kitendo hicho na kusakwa mtuhumiwa. “Niwaonye wananchi kwamba ukatili kama huu hauwezi kuvumiliwa, watu wajiepushenao maana watachukuliwa hatua za kisheria,” alionya Kamanda Wambura

0 comments:

WATOTO 22 WAFARIKI DUNIA HII NI BAADA YA KULA CHAKULA CHENYE SUMU SHULENI

Baadhi ya watoto hao wakipatiw huduma hospitalini jana.
Takribani watoto 22 wamekufa na wengine wengi wanaumwa baada ya kula chakula cha bure shuleni mchana ambacho kulichanganyika na dozi kubwa ya dawa za kuua wadudu, maofisa nchini India walisema jana.

Haikuweza kufahamika mara moja jinsi kemikali hizo zilivyoingia kwenye chakula hicho kwenye shule moja iliyoko mashariki mwa jimbo la Bihar, ingawa mmoja wa maofisa alisema inawezekana chakula hicho hakikuwa kimeoshwa vema kabla ya kupikwa.
Watoto hao, wenye umri wa kati ya miaka 8 na 11, walianza kuumwa juzi muda mfupi baada ya kula chakula cha mchana shuleni kwao huko Masrakh, kijiji kilichopo maili 50 kaskazini mwa mji mkuu wa jimbo hilo wa Patna.
Mamlaka za shule hiyo haraka zikasitisha kugawa chakula hicho cha wali, soya, dengu na viazi kufuatia watoto hao kuanza kutapika.
Chakula hicho cha mchana, sehemu ya kampeni maarufu ya nchi nzima kuwapatia chakula japo mlo mmoja watoto kutoka familia masikini, kilikuwa kimepikwa kwenye jiko la shule hiyo.
Watoto hao haraka walikimbizwa kwenye hospitali moja mjini humo na baadaye wakapelekwa Patna kwa matibabu, alisema msemaji wa serikali Abhijit Sinha.
Mbali na watoto hao 20 waliokufa, wengine 27 akiwamo mpishi wa shule walipelekwa hospitali, alisema. Kumi kati yao walikuwa katika hali mbaya.
Mamlaka zimemsimamisha kazi ofisa anayeshughulikia mpango wa mlo wa bure kwenye shule na kufungua kesi ya uzembe dhidi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo, ambaye alitoroka mara baada ya wanafunzi hao kuanza kuumwa.
P.K. Sahi, waziri wa elimu wa jimbo hilo, alisema uchunguzi wa awali umeonesha chakula hicho kilikuwa na kemikali ya organophosphate inayotumika kuulia wadudu kwenye mazao ya mpunga na ngano.
Inaaminika nafaka hiyo haikuwa imeoshwa kabla ya kupelekwa shuleni hapo, alisema.
Hatahivyo, wanakijiji walisema tatizo linaonekana kuwa upande wa chakula cha soya na viazi, wakaongeza kwamba watoto ambao hawakula chakula hicho walisalimika - ingawa walikula wali na dengu.
Mpango wa chakula cha mchana nchini India ni moja ya mipango mikubwa duniani ya lishe mashuleni.
Serikali za majimbo zina uhuru wa kuamua aina ya chakula na mida ya mlo huo kutegemea hali ya eneo husika na upatikanaji wa chakula hicho.
Kwa mara ya kwanza ilianzishwa kusini mwa India, ambako kulionekana kuwapo wazazi wengi mafukara wasio na uwezo wa kuwapeleka watoto wao shule.
Tangu hapo mpango huo umekuwa ukisambaa nchi nzima na kuwasikia zaidi wa watoto wa shule milioni 120 kama sehemu ya juhudi za kukabiliana na utapiamlo.
Kwa mujibu wa serikali hiyo, karibu nusu ya watoto nchini India wanasumbuliwa na utapiamlo.
Ofisa wa ngazi ya juu aliyechaguliwa wa Bihar, Waziri Mkuu Nitish Kumar, ameamuru uchunguzi ufanyike kuhusu vifo hivyo.
Chanzo zero99

0 comments:

MANDELA KUSHEREHEKEWA SIKU YAKE YA KUZALIWA LEO HUKU AKIWA MAHUTUTI HOSPITALINI :

Johannesburg: “Happy birthday Mzee Madiba.” Rais wa kwanza na mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, leo anatimiza umri wa miaka 95, pia anatimiza siku ya 40 tangu alipolazwa katika Hospitali ya Medclinic, Pretoria kwa ajili ya matibabu.
Nelson Rolihlahla Mandela, alizaliwa Julai 18, 1918 katika Kijiji cha Mvezo, eneo la Mthatha, Transkei Mkoa wa Eastern Cape na ametumia zaidi ya asilimia 70 ya maisha yake akipigania haki na usawa wa wananchi wa Afrika Kusini.
Maadhimisho ya miaka 95 tangu kuzaliwa kwa Mandela yanabeba uzito mkubwa kuliko maadhimisho mengine yaliyotangulia kwani kwa siku 40, wananchi wa Afrika Kusini wamekuwa katika wasiwasi mkubwa hasa kutokana na kuzorota kwa afya ya kiongozi huyo.
Mandela alilazwa katika hospitali hiyo Juni 8, mwaka huu akiugua magonjwa ya figo na afya yake imeelezwa kuwa ni mbaya.
Leo, Rais Jacob Zuma atawaongoza mamilioni ya wananchi wa Afrika Kusini katika maadhimisho ya nne ya kimataifa ya ‘Siku ya Mandela’ ambayo yanakwenda sambamba na siku yake hiyo ya kuzaliwa.
Tangu kulazwa kwa Mandela huko Pretoria, Rais Zuma amekuwa akiwahimiza wananchi wake wajiandae kusherehekea miaka 95 ya Mandela akiwatia moyo wale waliokuwa na wasiwasi kwamba Madiba asingeweza kuifikia leo kutokana na matatizo ya kiafya.
Siku ya Mandela huadhimishwa kuenzi kazi za kiongozi huyo alizozifanya kwa miaka 67 akiutumikia umma wa wananchi wa Afrika Kusini, zikiwamo vita dhidi ya ubaguzi wa rangi na hatimaye kuwa Rais wa kwanza mzalendo kwa miaka mitano, kisha kustaafu.
Pia ‘Mandela Day’ hutumika kukumbuka kampeni yake dhidi ya ubaguzi wa rangi na utetezi wa haki za binadamu maarufu kwa jina la “46664”, ambayo ni namba ya utambulisho aliyoitumia alipokuwa mfungwa katika Gereza la Visiwa vya Robben.
Dakika 67 za Mandela
Kwa maana ya Siku ya Mandela ambayo pia imeidhinishwa na kutambuliwa na Umoja wa Mataifa, wananchi wa Afrika Kusini wanatumia dakika 67 kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwa ni hatua ya kuenzi kile wanachokiita ‘kazi za mtu aliyejitoa maisha yake kwa ajili ya kupigania haki na utu’.
Dakika hizo 67 zinawakilisha idadi kama hiyo ya miaka ambayo Mandela alitumika, hivyo Waafrika Kusini watakuwa wakitoa msaada na huduma kwa jamii iwe ni kwa watoto yatima au watu wengine ambao ni wahitaji katika jamii.
Kituo cha Kumbukumbu ya Mandela kimewataka wananchi kuungana na kuonyesha ushirikiano wao kwa Mandela kwa kutumia dakika 67 za muda wao kuzisaidia jamii zao ili kumuenzi kiongozi huyo ambaye ni alama ya dunia

0 comments:

HIZI NDIO TOFAUTI KATI YA MADEMU WA UDSM NA MADEMU WA UDOM :SOMA HAPA UJUE CHUO GANI WANAFUNIKA:



Kuna tofauti kubwa kati ya mabinti wa UDSM na wale wa UDOM. Mbali na kwamba wote ni wazuri na wamemeenda vidato lakini zipo tofauti kubwa baina yao zinazowatofautisha. Kwa ujumla tofauti zao ni hivi zifuatazo;

Muonekano (image)
Binti wa UDSM mara nyingi atapenda avae vitu mpaka aonekane kama mwanamitindo. Atajiwekea make up za kila aiana japokuwa tayari ana uzuri natural. Atataka avae fasheni mpya mpya zinazotokana kwa kuwa yuko town na mara nyingi hata kama boom haliruhusu kuna wananchi wengi wa kuwapiga mizinga.  Nguo zao wananunulia Mlimani City, Quality Center, Makumbusho, Mwenge kwa White na maeneo mengine kama hayo.  Jinsi wanavyovyaa unaweza ukawaogopa kudhani ni expensive saaaaana.
Binti wa UDOM kwa upande mwingine anavaa kawaida tu. Viatu vyake vya mchomekeo wanavinunua pale SabaSaba lakini waulize wavulana UDOM sasa, watakwambia binti katoka bomba yule si mchezo. Viatu vyao ni bei za kawaida na huvumilia hali zote za hewa. Huwa shopping zao wanafanya Saba Saba. 


Sehemu ya kuangalia movie (cinema)
UDSM huwezi kumpeleka binti kucheka movie room kwako! Sijui eti Hall 3 au ghetto Survey! Utampeleka Suncrest Quality Center au Mlimani City na hapo uweke bajeti ya PopCon na mazagazaga kibao ya kucheki cinema.
Binti wa UDOM wewe tu na laptop yako unamkaribisha chumbani Block 9, 10, etc maeneo ya Haiti mnacheki movie huku mkinywa maji ya kudownload, bites za Discount shop au chai. Umemaliza.
Sehemu ya kukutania (Date location)
Kama unadhani binti wa UDSM utampeleke room yako namba 2409 kule Hall 3 sahau! Kama huna ghetto la ukweli Survey au Sinza au Ubungo Maziwa au unamiliki nyumba kabisa jua imekula kwako. Sehemu ya kukutania lazima iwe ya kueleweka na treatment isomeke vizuri kama misosi iliyosimama, Pizza, Burger, Chicken Chips, etc. Hapo lazima Bamaga upajue vizuri, Mikocheni na Sinza. Kishushio Savanna au Red Bull. Mjomba huna hivyo UDSM utawapata wa kuhesabu kukusikiliza maelezo yako ya kuunga unga.
Binti wa UDOM yeye hata hajali. Wewe tu, uwe kule porini mnapaita Ng’ox au Social Room kwako atakuja. Mtengenezee chai kwa ule mkate wako wa juzi halafu anza kumwaga point zako. Huna haja ya kupajua Area D, Area C wala Lodge za Area A ila ukikosea ukakuta mwenye kaupepo ka jiji lazima kuku wa Club Maisha na 84 ujue bei yake.

Upatikanaji wao (Availability)
Binti wa UDSM atakuona akitaka kukuona si kinyume chake. Ukimpigia simu mkutane atakupa sababu kibao utabaki kichwa kinakuuma ila yeye akikupigia simu mkutane hataki kusikia sababu yako hata moja. Anapenda yeye awe na control.
Binti wa UDOM yeye anaelewa principle ya give and take vizuri sana. Anaelewa mla lazima aliwe na anaelewa ili uhusiano uwepo lazima kila mtu aplay part yake.  Ukimpigia simu baada ya dakika au saa chache utamuona na wanapenda kutembea na wavulana wao campus. Kama unabisha angalia idadi ya mabinti wa UDSM wanaotembea na boys ndani ya campus na wale wa UDOM wanaofanya hivyo ndani ya campus.
Mtazamo wao kuhusu mapenzi (Perception of love)
Binti wa UDSM atakupenda kwa ile ulichona nacho. Kichwa class, una hela au famous. Nje ya hapo ni wa kuhesabu bro.
Binti wa UDOM atakupenda jinsi ulivyo hasa kama shule kasoma Songea huko kwao vijijini chuo katua Dodoma, ila ukikuta ana kahewa ka Dar kidogo lazima utasanda. Yale yale.

Mwandishi wa Makala hii amejitambulisha kuwa ni mhitimu wa Digrii ya Ukandarasi na sasa ni chizi hospitali ya Lutindi Tanga.

SOURCE: ORIGINAL K

0 comments:

WANASAYANSI WAGUNDUA NJIA ZA KUCHAJI SIMU KWA MKOJO


Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji betri za simu, na kudai kuwa wa kwanza kutengeneza “the world’s first microbial fuel cells (MFC) powered mobile phone”.
 

Watafiti hao walielezea juu ya ugunduzi wao kupitia jarida la ‘Physical Chemistry Chemical Physics’.
Dr Ioannis Ieropoulos amesema, huo ndio ugunduzi wa kwanza wa kuzalisha nguvu ya umeme kwa kutumia mkojo, na katika majaribio ya utafiti huo wamefanikiwa kuchaji simu ya Samsung.
 

Wanasayansi hao wanaamini kuwa teknolojia yao inaweza kutumika katika mabafu huko mbeleni kwaajili ya kuwashia mashine za kunyolea au kupasha moto maji ya kuoga na kuwasha taa

0 comments:

Tendwa hana ubavu wa kuifuta Chadema

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, hana mamlaka yoyote ya kukifuta chama hicho.

Mbowe amesema kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwataka wananchi wadai haki zao nje ya utaratibu rasmi, jambo alilosema ni la hatari kwa ustawi wa taifa.

Aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya malori iliyopo katika eneo la Majengo mjini hapa na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa Manispaa ya Songea na mikoa jirani ya Lindi na Mtwara waliofika  kushuhudia uzinduzi wa Kanda ya Kusini ya chama hicho.

Mbowe alisema kuwa binadamu yeyote pale anapodai haki yake, hapaswi kuzuiwa katika mazingira tatanishi, hivyo wanachama wa Chadema wana haki ya msingi ya kujiwekea ulinzi wao (Red Brigade) kama wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walivyojiwekea ulinzi wao kupitia vikundi vya Green Guard na si vinginevyo.

Alisema kuwa suala la Red Brigade siyo geni na wala halijaanzishwa na Mbowe, bali limewekwa bayana kwenye Katiba ya Chadema tangu mwaka 2006 ambapo linasema chama kitajiwekea ulinzi wa mali na viongozi wao, hivyo kuifuta Chadema ni kutafuta machafuko ndani ya nchi.

Mbowe alimtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuona umuhimu wa kuweka miundombinu ya kuwa na amani kwa kusimamia kikamilifu haki kwa vyama vyote vya siasa vilivyopo hapa nchini badala ya kuwa na upendeleo kwa CCM ambacho kinaonekana kuwa na propaganda nyingi kandamizi za kisiasa.

Alisema kuanzia sasa, Chadema itahakikisha kuwa inakuwa na ulinzi mkali kwa kuweka vikundi vya Red Brigade ambavyo vitakuwapo katika ngazi za serikali za mitaa, vijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa.

Alifafanua kuwa kazi za vikundi hivyo itakuwa ni kulinda usalama wa mali za chama pamoja na viongozi wao.

"Red Brigade ilikuwapo tangu awali isipokuwa kwa hivi sasa kilichofanyika ni kuiongezea uwezo ambao umevifanya vyombo vya dola vishtuke na kuanza kuipigia Chadema kelele ingawa majukumu yake ni yale yale na yanaelekeana na vikundi vya Green Guard vya CCM.

Hata hivyo, Mbowe alisema kuwa vikundi vya  Green Guard vya CCM vimekuwa vikifanya matukio mengi ya kihalifu, lakini Jeshi la Polisi limekuwa likiyafumbia macho.

Alisema anayo mifano ya matukio ya uhalifu ya vikundi vya Green Guard, hakuyataja na kueleza kuwa wahalifu walikamatwa, lakini wakatoroshwa katika mazingira yenye utata.

Kuhusu rasimu ya Katiba, Mbowe amewahimiza wananchi kuwa makini anapoijadili.

Hata hivyo, alisema CCM inataka kuweka taratibu inazozitaka wakati Tume ya Katiba iliandaa vizuri, hivyo Chadema nayo ina mpango wa kuwa na tume yake ya kuijadili rasimu hiyo kwa kuwaelimisha wananchi mambo halisi yanayopaswa kuwapo katika Katiba mpya.      chanzo:chadema blog.

0 comments:

MFAHAMU MTU MREFU KULIKO WOTE DUNIANI.HUYU HAPA

Sultan Kosen MTU MREFU KULIKO WOTE DUNIANI



  

0 comments:

MAMA YAKE BAGHADAD AMUANGUKIA CHID BENZ AMUOMBA WAMALIZE TOFAUTI NA MWANAYE.STORI NZIMA HII HAPA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXrZGSuwtDKT9hSwi9TCpGNDA09HDY-ZAWtzpEI2dAJmAk5iCWvnIxpGFcrjNIZSx2QFKrQqYs-FzgYt0A-uvfgCiGMXZcDmGeMt0SX2ld6GdRzQaiFN485aArUOhBCPmlBkDeM4ikhtM/s320/ch.jpg
Baada ya jana Chidi Benz kuweka wazi kuwa hategemei kumsamehe Baghdad kwa ‘blunder’ aliyoifanya ya kuwashirikisha yeye na Nay wa Mitego bila kuwaambia, mama mzazi wa Baghdad amekuja hadharani na kumuombea msamaha mwanae.
Mama huyo ameongea leo kwenye segment ya 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kuhusu nia yake ya kutaka kumaliza tofauti zilizopo kati ya mwanae na Chidi.

Mama Baghdad amekiri kuwa mwanae hakutumia akili kuchukua uamuzi huo wa kuwashirikisha wasanii wanaofahamika kuwa na uadui mkubwa kimuziki bila kufikiria madhara yake.

Amesema mwanae hakufanya jambo la busara na ndio maana ameamua kumpigia magoti Chidi ili ampe ‘second chance’ mwanae ambaye amejaribu kuomba msamaha bila mafanikio.

255 pia imezungumza na Chidi Benz aliyepo nchini Kenya kwa sasa ambaye amesema hawezi kukataa wito wa mama yake na Baghdad kwakuwa ni kama mama yake pia na amekubali kuja kukutana naye akirejea nchini.

Jana wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya, Chidi alisema kamwe hatokuja kumsamehe Baghdad. 

Source:Mambo Mseto {Radio Citizen},Kenya

0 comments:

SOMA HAPA NI KUHUSU PREZZO KUKATAA KUMUOMBA MSAMAHA DIAMOND PLATNUMZ KUPITIA TWITTER.STORI NZIMA HII HAPA




Rapcellency, Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kwakuwa anaamini hakuna alichomkosea na ni jambo la kitoto.
 Akiongea jana  mchana kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen, kinachoendeshwa Mzazi Willy M. Tuva, Prezzo amesema Diamond ndiye aliyemchokoza baada ya wasanii hao kutumbuiza mwanzoni mwa mwezi huu kwenye tamasha la Matumaini.

 Prezzo anadai aligundua kuwa Diamond alimponda kwenye magazeti ya Tanzania kuwa hamwezi kwa lolote kwenye muziki.

“Mimi sipendi kuwa na adui kwa sababu muziki unafaa kuleta muungano, sa me nikashangaa mbona huyu brother ananiingilia na huku sikumbuki kumkosea wala hatujawai kukutana ana kwa ana,” alisema Prezzo.
 
“Mtu yeyote anamjua Prezzo ni kama rattle snake, ukimchokoza you have to get prepared to be bitten.”
 Rapper huyo aliendelea kudai kuwa alimpigia simu Diamond lakini hakupokea na ndio maana aliamua kumdiss kwenye Twitter.
  “Jamaa hakupokea simu nikaona ah! Basi liwalo na liwe, nikadecide ku-air my views.”
Hata hivyo Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kama anavyomtaka afanye.
 
 “Unaona kwa saa hizi akianza kusema aende kwa Twitter aniombe msamaha, maisha huwa hayaendi hivo…kwa hivyo vitu vingine naona ni kama ni utoto unaingilia kati, kwani yeye kusema niombe msamaha kwa Twitter….niombe msamaha kwa kosa gani? Kusema ukweli,unajua mimini msema ukweli, mimi kuomba msamaha kwa Twitter naona kidogo ni utoto.”
Hata hivyo Prezzo amesema hataki beef na Diamond kwasababu anamheshimu na amemshukuru Willy Tuva kwa kujaribu kuwasuluhisha.

0 comments:

PICHA 5 ZA WANAJESHI WA TANZANIA WALIO UAWA DARFUL WAAGWA


Kapteni John Kivunge, Wafanyakazi wa Tanzania Afisa Joc, wasomaji mpango wa sherehe fupi.
 
Sala kutoka kwa mchungaji.
 
Maombi kutoka kwa Imamu kwa walinzi wa amani wa waasi.

 .. 
Kijeshi salute kama pete 'Last Post' nje na Nigbatt kwa heshima ya mashujaa imeanguka

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz