DUDE APATA AJALI LOLIONDO

STAA wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ amepata ajali ya gari wakati akielekea Loliondo, Arusha kupata dawa ya kikombe inayotolewa na mchungaji mstaafu, Ambilikile Mwaisapila.



Staa wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’

Dude ameiambia Bongowood kuwa, hivi karibuni walikuwa na gari aina ya Toyota Prado wakimpeleka mama yake kupata tiba ya ganzi mwilini ndipo tairi lilipopasuka na gari kuangukia gema.

“Ilipoteza muelekeo, likayumba lakini nashukuru Mungu hatukuumia, tukasaidiwa kunyanyua, tukaenda kupata tiba ya babu,” alisema Dude.

NA GPL

0 comments:

MAMA SHARO MILIONEA AMVAA KITALE KWA TUHUMA NZITO NA ZA AIBU...!


Mama yake na marehemu Hussein Mkieti aka ‘Sharo Milionea’ .Makubwa! Mama mzazi wa aliyekuwa nyota wa filamu na muziki, marehemu Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’ amemtuhumu msanii wa vichekesho ambaye alikuwa rafiki wa mwanaye, Musa Kitale kuwa alikula michango ya kumbukumbu ya kifo cha mwanaye, mwaka jana.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Mama Sharo amekuwa akimlalamikia Kitale kwa watu kwamba alikula fedha za mchango wa mwanaye hivyo kupigwa marufuku kwamba kitu chochote kinachomhusu Sharo asipewe.
Ilidaiwa kwamba, chanzo cha mama Sharo kutaka Kitale asipewe kitu chochote kinachomhusu marehemu ni baada ya hivi karibuni Klabu ya Bongo Movie Unity kutangaza kuwa litatoa Tuzo kwa Sharo Milionea kama kumbukumbu kwani alikuwa ni mwenzao katika tasnia ya filamu.
Ilisemekana kuwa mama huyo alielezwa kwamba tuzo hiyo itapokelewa na Kitale ndipo alipokataa na kusema hataki kabisa kitu chochote kipitie kwa msanii huyo kwa sababu huwa hamfikishii.


Msanii wa vichekesho Musa Kitale.“Mama Sharo amekuwa akilalamika kwa muda mrefu sana kwamba Kitale anatumia vitu vya mwanaye, eti alichangisha michango ya kumbukumbu hakumfikishia hivyo kwa sasa ameamua kupiga marufuku asikabidhiwe kitu chochote,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya kupata habari hizo, wanahabari wetu walimtafuta Kitale ambapo kabla hata ya kujibu tuhuma hizo, alinyanyua simu na kumpigia mama Sharo kumuuliza kama kweli amezungumza madai hayo.
Mama Sharo alikiri kuwa ni kweli alizungumza akidai alifikia uamuzi huo baada ya kutonywa na watu kuwa Kitale amekuwa ‘akichikichia’ fedha za marehemu mwanaye.
Kitale, baada ya kujiridhisha, alitoa ufafanuzi kuwa madai hayo hayana ukweli na kudadavua kwamba wakati wa kumbukumbu ya Sharo mwaka mmoja (Novemba) tangu alipofariki dunia, hakuna michango yoyote iliyotolewa.
“Inaniuma sana kwa sababu enzi za uhai wa Sharo hatukuwahi kugombana hata siku moja na mama Sharo alikuwa analitambua hilo, tuliishi kama ndugu na mimi ndiye niliyemsaidia mpaka akapata umaarufu lakini sasa namshangaa huyu mama kunishutumu vitu vya uongo,” alisema Kitale kwa huzuni huku jasho likimtiririka.
source: kiuyahaki blog

0 comments:

Mwandishi Uingereza aibua mapya meno ya tembo Tanzania







Mwandishi wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, Martin Fletcher akiwa katika chumba cha kuhifadhi meno ya tembo katika Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam ambako zaidi ya meno 34,000 yamehifadhiwa. Picha ya Daily Mail.
Na Mwandishi Wetu, Mwananchi


Mwandishi huyo anaripoti kuwa; “Wahisani ambao wangeweza kutoa fedha hizo, walikejeli kiwango hicho wakisema hakina uhalisia.”


Dar es Salaam. Licha ya Rais Jakaya Kikwete kutoa ahadi ya kuteketeza maelfu ya meno ya tembo yaliyo kwenye ghala la Serikali, imeelezwa kuwa uwezekano huo ni mdogo.


Mwandishi wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, Martin Fletcher ameeleza kushtushwa na hali ya ulinzi kwenye ghala hilo lililosheheni meno 34,000 ya tembo ambayo kwa biashara ya magendo nchini China yanagharimu Pauni 150 milioni za Kiingereza (Sh403.5 bilioni)


Fletcher, ambaye aliandika habari ya kuhusika kwa wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa wa Tanzania katika biashara haramu ya meno hayo kiasi cha kuifanya nchi kuwa muuzaji mkuu wa nyara hizo, aliandika hayo kwenye taarifa kuhusu ziara yake nchini iliyochapishwa na gazeti hilo jana.


Habari ya awali ilitikisa ulimwengu ambao unapambana kulinda viumbe walio hatarini kutoweka ikiwatuhumu wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa nchini kuhusika, huku Serikali ikishindwa kuwadhibiti.


Habari hiyo iliifanya Serikali ya Tanzania kufungua milango kwa vyombo vya habari vya nje kuja nchini kupata habari sahihi kuhusu tatizo hilo, akiwamo Fletcher wa Daily Mail.


Katika ziara yake, Fletcher alipata nafasi ya kutembelea ghala la nyara hizo, kuzungumza na maofisa wanyama pori pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.


“Nyalandu pia aliweka bayana kuwa uteketezaji wa shehena ya Tanzania ni kitu ambacho kiko mbali na uhalisia, licha ya ahadi ya Kikwete jijini London,” Fletcher alimkariri Nyalandu kwenye habari hiyo ambayo imeambatana na picha alizozielezea kuwa za kushtua za ghala hilo, lenye idadi kubwa ya meno ya tembo kuliko maghala yote duniani.


“Alisema Rais alikuwa na nia ya kuteketeza (shehena hiyo), lakini Tanzania ilitaka ilipwe takriban Pauni 30 milioni za Uingereza kutoka Jumuiya ya Kimataifa kwa ajili ya Mfuko wa Hifadhi ya Tembo.”





Hata hivyo mwandishi huyo anaripoti kuwa; “Wahisani ambao wangeweza kutoa fedha hizo, walikejeli kiwango hicho wakisema hakina uhalisia.”


Alipoulizwa kuhusu kauli hiyo jana, Nyalandu alisema baadhi ya mambo kwenye habari ya mwandishi huyo yamekuzwa, lakini alisema uamuzi wa kuteketeza nyara hizo haujafikiwa.


Alisema Serikali ilichofanya hadi sasa ni kupiga marufuku biashara zote za meno ya tembo, hivyo haitauza yaliyopo na haitaomba kibali tena cha kufanya biashara hiyo na kwamba kinachoendelea sasa ni mazungumzo ya namna ya kushughulika na shehena iliyopo.





“Meno mengine yaliyopo ni ya kihistoria. Ni marefu kuliko mengine na tembo wa aina hii hawapo tena, hivyo kuwa nayo pia ni kitu kizuri. Haya meno ni mali ya Watanzania wote, uamuzi wa kuyateketeza lazima uchukuliwe kwa busara,” alisema.


Kwa mujibu wa Fletcher meno mengine yana urefu wa futi 7, uzito wa tani 125 na moja linaweza kubebwa na watu kuanzia watatu, huku jino fupi likiwa na uzito wa kilo 0.4500 na kwa mujibu wa jangili aliyekiri kuua tembo 30 kwa siku, jino hilo dogo liling’olewa kutoka kwa tembo mtoto.


Mara tatu katika kipindi cha miaka minane, Tanzania imeomba bila mafanikio kibali cha kuuza shehena yake kutoka katika nchi 180 zilizosaini makubaliano ya kudhibiti biashara ya kimataifa ya viumbe walio hatarini kutoweka, Cites, licha ya ushahidi mkubwa kuwa kitendo cha kuuza mara moja tu, kitazidisha tamaa ya China kupata meno hayo.


Akizungumzia ziara yake nchini, mwandishi huyo anaelezea udhaifu katika ulinzi wa ghala hilo lililo nyuma ya jengo la Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam.


“Ghala hilo niligundua siyo kama ngome (yenye ulinzi mkali). Lina milango ya chuma ya kusukuma ikiwa na kufuli nzito tano ambazo funguo zake zimegawanywa kwa maboharia wawili, lakini milango ilifunguliwa yote nilipofika,” makala hiyo inaeleza. “Kila jino limewekwa alama na namba na ghala ina kamera za ulinzi wa ndani, lakini sikuona mlinzi mwenye silaha nje.”


Mwandishi huyo anaeleza kuwa habari yake ya kwanza iliyohoji kama mtoto wa Mfalme wa Wales na Waziri Mkuu wanaweza kushikana mkono na Rais Kikwete wakati alipotembelea Uingereza, ilizua kizaazaaa kiasi cha Rais Kikwete kuitisha kikao na maofisa waandamizi wa Maliasili na kutoa maelekezo kuwa wafanye kazi.


Mwandishi huyo alitembelea maghala ya meno ya tembo, Hifadhi ya Selous ambayo mwaka 2006 ilikuwa na tembo 70,000 lakini hadi sasa wamesalia 13,000 tu. Baadhi ya meno yalichukuliwa kutoka tembo waliokufa na mengi kukamatwa kutoka kwa majangili na hayawezi kuuzwa kwa sababu ya biashara hiyo kuzuiwa duniani.

0 comments:

Kijana akamatwa kwa mauaji London





Shereka Fab-Ann Marsh msichana mwenye umri wa miaka 15 aliyeuawa

Kijana mwenye umri wa miaka 15, amefikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji mjini London Uingereza.

Kijana huyo alimuua msichana Shereka Fab-Ann Marsh mwenye umri wa miaka 15 katika mtaa wa Hackney siku ya Jumamosi.

Polisi wamesema kuwa msichana huyo alifariki katika nyumba moja mtaani humo saa kumi Jioni.

Kadhalika Kijana huyo ambaye ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu ya umri wake mdogo, anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.

Vijana wengine wawili waliokamatwa kuhusiana na mauaji hayo, wameachiliwa na polisi

0 comments:

Waponea kifo mikononi mwa Boko Haram





Jeshi linaendelea kuwasaka wapiganaji wa Boko Haram

Wasichana waliotekwa nyara na kundi lenye itikadi kali za kidini, Boko Haram nchini Nigeria, wameielezea BBC ukatili walio upitia mikononi mwa kundi hilo.

Wakati wakizuiwa, wasichana hao walishuhudia watu kadhaa wakiwemo baadhi wanaotoka kijiji kimoja na wapiganaji wa kundi hilo, wakikatwa shingo.

Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 23, ameiambia BBC kwamba ameona kiasi ya raia hamsini wakiuawa mbele yake na Boko Haram.

Hili limefanyika miezi kadhaa iliyopita katika kambi moja katika eneo la mashambani, la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Wakati huo huo msichana mwingine alieleza jinsi wapiganaji hao walivyo mlazimisha kumuua mwenziwe ambaye pia alitekwa nyara.

Wote walifanikiwa kutoweka kutoka kambi hizo na sasa wanaishi mafichoni.

Jeshi la Nigeria linasema linaendelea kuwasaka wapiganaji wa kundi la Boko Haram katika eneo hilo lililo mashinani.

Wapiganaji hao wanaendelea kuyashambulia miji na vijiji katika kiwango cha kushtusha ambapo zaidi ya raia mia tano wameuawa katika wiki za kwanza za mwaka huu.

0 comments:

Siri ya papai kwa urembo wako







0 comments:

Wale wa Yanga – hiki ndio kikosi cha Yanga kilichotangazwa kucheza leo na Rhino

yanga-16

Muda mchache ujao mabingwa watetezi wa VPL Yanga wanajitupa katika dimba la Al Hassan Mwinyi mjini Tabora kupambana na Rhino Rangers, millardayo.com imebahatika kupata kikosi cha Yanga cha leo na kipo kama ifuatavyo:

0 comments:

TAJIRI WA MAFUTA,MWARABU WA DUBAI, AHAIDI KUMHONGA ELIZABERTH MICHAEL GARI NA HEKALU SOMA HAPA









0 comments:

SHEIKH PONDA ARUDISHWA SEGEREA, MAHAKAMA YATUPILIA MBALI OMBI LA DHAMANA YAKE


Ombi la marejeo lililowasilishwa na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda limetupiliwa mbali na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam
ilipotoa uamuzi wa pingamizi la awali lililowasilishwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), akidai kuwa ombi hilo halikuwa na msingi kisheria.
 
Kesi hiyo iliyosikilizwa kwa saa 1 na dakika 40 ilitolewa uamuzi na Jaji Augustine Mwarija.
Baada ya uamuzi huo, Sheikh Ponda alirudishwa jela huko Segerea jijini Dar akiwa chini ya ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi. 
Via GPL

0 comments:

Biashara: Jeshi la Polisi lakamata kiwanda cha kutengeneza Konyagi feki

0 comments:

Jux - Uzuri Wako (Official Video)

0 comments:

SOMA: Nikki Wa Pili atoa tamko: Baada ya habari za kukamatwa kwa tuhuma za wizi Arusha, Weusi wamsimamisha Lord Eyes


Msanii na msemaji mkuu wa Weusi Nikki wa Pili, ametoa tamko juu ya msanii mwenzao Lord Eyes na kusema kuwa kampuni kama kampuni imemsimamisha Lord Eyes na kwa yeyote anaetaka kujua habari zake amtafute Lord mwenyewe.

0 comments:

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI: MAUWAJI YA KINYAMA YATOKEA KAHAMA


0 comments:

Kutoka Bunge Maalum La Katiba Mjini Dodoma





Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Christopher Ole Sendeka akichangia mjadala kuhusu vifungu vya kanuni vitakavyotumika katika Bunge Maalum la Katiba.

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz