Angalia hapa mitindo mbali mbali ya mavazi





0 comments:

Wandishi wa BBC washambuliwa Urusi


BBC imeitaka serikali ya Urusi kuchunguza tukio hilo dhidi ya wandishi wake

BBC imewasilisha malalamiko kwa serikali ya Urusi baada ya wandishi wake wa habari kushambuliwa Kusini mwa nchi hiyo.

Wandishi hao walikuwa nchini Urusi kuchunguza madai ya baadhi ya maafisa wa usalama wa Urusi kuuawa karibu na mpaka na Ukraine.

Baada ya kuwaarifu maafisa wa huduma ya dharura , waandishi hao walipelekwa katika kituo cha polisi na kuhojiwa kwa saa nne.

Picha walizokuwa wamenasa kwenye kamera zilifutwa wakati wakiwa kwenye kituo cha polisi.

BBC inasema kuwa imechukizwa na kitendo hicho na kutoa wito kwa maafisa wa utawala nchini humo kuchunguza taarifa hizo pamoja na kuwataka kulaani kitendo hicho.

0 comments:

Scotland yaamua kuhusu muungano

Wascochi wanapiga kura kuamua ikiwa wataendelea kuwa sehemu ya Uingereza au watajitawala

Wapiga kura wamekuwa wakielekea kwa vituo vya kupigia kura katika maeneo mbali mbali nchini Scotland, ambapo watu wanaamua leo ikiwa wataendela kuwa sehemu ya uingereza au wawe taifa huru kwa mara ya kwanza kabisa tangu zaidi ya miaka 300 iliyopita.

Mwandisi wa bbbc anasema kuwa siku ya leo inatarajiwa kuwa ya shughuli nyingi katika historia ya kupiga kura eneo la Scotland ikiwa asilimai 97 ya watu wamejisajili kupiga kura.

Kumekuwa na kampeni kali katika saa 24 zilizopita huku ikidhihirika matokeo yanaweza kwenda upande wowote.

Kiongozi wa chama cha Scotish National Party, Alex Salmond, ametaja kampeni ya kuitisha Uhuru wa Scotland kutoka kwa Uingereza kama tukio muhimu zaidi la kidemokrasia kuwahi kutendeka nchini humo.

Kadhalika amesema tayari limebadilisha mfumo wa maisha eneo la Scotland.

Idadi kubwa ya wapiga kura wamesajiliwa na kwa mara ya kwanza vijana wenye umri wa miaka 16 na 17 wataruhusiwa kupiga kura.

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz