BBC imeitaka serikali ya Urusi kuchunguza tukio hilo dhidi ya wandishi wake

BBC imewasilisha malalamiko kwa serikali ya Urusi baada ya wandishi wake wa habari kushambuliwa Kusini mwa nchi hiyo.

Wandishi hao walikuwa nchini Urusi kuchunguza madai ya baadhi ya maafisa wa usalama wa Urusi kuuawa karibu na mpaka na Ukraine.

Baada ya kuwaarifu maafisa wa huduma ya dharura , waandishi hao walipelekwa katika kituo cha polisi na kuhojiwa kwa saa nne.

Picha walizokuwa wamenasa kwenye kamera zilifutwa wakati wakiwa kwenye kituo cha polisi.

BBC inasema kuwa imechukizwa na kitendo hicho na kutoa wito kwa maafisa wa utawala nchini humo kuchunguza taarifa hizo pamoja na kuwataka kulaani kitendo hicho.
Wascochi wanapiga kura kuamua ikiwa wataendelea kuwa sehemu ya Uingereza au watajitawala

Wapiga kura wamekuwa wakielekea kwa vituo vya kupigia kura katika maeneo mbali mbali nchini Scotland, ambapo watu wanaamua leo ikiwa wataendela kuwa sehemu ya uingereza au wawe taifa huru kwa mara ya kwanza kabisa tangu zaidi ya miaka 300 iliyopita.

Mwandisi wa bbbc anasema kuwa siku ya leo inatarajiwa kuwa ya shughuli nyingi katika historia ya kupiga kura eneo la Scotland ikiwa asilimai 97 ya watu wamejisajili kupiga kura.

Kumekuwa na kampeni kali katika saa 24 zilizopita huku ikidhihirika matokeo yanaweza kwenda upande wowote.

Kiongozi wa chama cha Scotish National Party, Alex Salmond, ametaja kampeni ya kuitisha Uhuru wa Scotland kutoka kwa Uingereza kama tukio muhimu zaidi la kidemokrasia kuwahi kutendeka nchini humo.

Kadhalika amesema tayari limebadilisha mfumo wa maisha eneo la Scotland.

Idadi kubwa ya wapiga kura wamesajiliwa na kwa mara ya kwanza vijana wenye umri wa miaka 16 na 17 wataruhusiwa kupiga kura.



Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wanatarajiwa kumaliza bonanza liloanza siku ya jumatano chuoni hapo 
Akizungumza na BLog hii kwa nyakati tofauti mwalimu wa michezo chuoni hapo amesema kuwa mashindano yaliyoandaliwa na kamati ya michezo yana malizika leo.
Baadhi ya michezo iliyokuwamo ni mpira wa miguu,netball,kucheza karata,kula,kuzunguka viti,kucheza draft na mingine mingi.Alisema lengo ni kutafuta timu bora ya chuo pamoja na kuwafanya wanafunzi kuwa vizuri kiafya na kiakili kwani michezo hujenga mwili kwa kufanya mazoezi.
Pia waalimu wa chuo hicho walihusishwa kwenye mashindano hayo kwa kupewa dhamana ya kuwa marefa kwenye mpira wa miguu pamoja na netball.
Wanafunzi wa chuo hicho walionyesha ushirikiano mzuri kwa kuwashabikia wenzao walipokuwa wakicheza.
Zawadi za washindi wote kwa ujumla zitatolewa leo chuoni hapo baada ya kumalzika kwa michezo yote...



MBUNGE wa Urambo Magharibi, Prof. Juma Kapuya (CCM), ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi wa zamani, jana alijikuta katika wakati mgumu wa kuumbuliwa na mbunge mwenzake wa Temeke, Abbas Mtemvu (CCM), wakati wawili hao wakibishania uuzwaji tata wa Kampuni ya Usafiri Dar es Salaam (UDA).Hatua hiyo ilijitokeza wakati Mtemvu akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa mwaka wa fedha 2014/2015, na kuungana na wabunge wenzake kadhaa waliotangulia kuchangia, akidai UDA imeuzwa kifisadi bila wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam kushirikishwa.
 Wakati Mtemvu akiendelea kujenga hoja yake, Prof. Kapuya aliomba kumpa taarifa, akimweleza kuwa mbunge kujishughulisha na uwekezaji si dhambi na kwamba UDA imeuzwa kihalali wala hakuna ufisadi kama inavyodaiwa, isipokuwa mbunge huyo anatumika kuwashawishi wabunge kupinga suala hilo. Baada ya Prof. Kapuya kuketi,



Mtawa wa Italia anyakua ushindi
Mtawa mmoja kutoka Italia ambaye alipata umaarufu katika mtandao wa kijamii ameshinda shindano la kuimba nchini humo.
Mtawa huyo, Sister Christina Scuccia alitokea kwa mara ya kwanza katika televisheni kushiriki shindano la The Voice.
Scuccia aliyeonekana amevalia mavazi yake ya utawa na msalaba shingoni, alijawa na furaha na kumshukuru Mungu kwa kumfikisha katika ushindi huo.
Mtindo wake wa wimbo wa Alicia Keys, kwa jina 'No One', umetizamwa zaidi ya mara milioni 50 katika mtandao wa You Tube tangu auimbe.
Mtawa huyo mwenye umri wa miaka 25 amesema kuwa aliamua kushiriki mashindano hayo kufuata ushauri wa Papa mtakatifu Francis, kuwa kanisa liwakaribie zaidi watu wa kawaida.

wanawake wa Misri
Kwa mara ya kwanza Misri imepitisha sheria inayotaja unyanyasaji wa wanawake kuwa uhalifu.
Chini ya sheria hiyo wanaume watafungwa miaka 5 gerezani kwa kuwanyanyasa wanawake hadharani au faraghani.
Sheria hiyo imepitishwa kama hatua ya mwisho kuchukuliwa na rais anayeondoka wa Misri Adly Mansour.
'Unyanyasaji umezidi'
Watetesi wa haki za wanawake nchini Misri wamesema kuwa unyanyasaji wa wanawake umefikia viwango vya kuhuzunisha. Utafiti uliofanywa umeonesha kuwa karibu wanawake wote wa Misri wamewahi kupitia unyanyasaji wa aina fulani iwe ya matusi au hata ubakaji.
Utafiti huo umeonesha kuwa hata mavazi ya kufunika mwili wote yanayopendekezwa na sheria za kiislamu nchini humo, hazijawazuia wanaume hao kuwanyanyasa wanawake.
Na sasa inahofiwa kuwa mapinduzi waliofanya mwaka wa 2011 hayakuleta mabadiliko yoyote.
Wanawake wengi wamelalamika kuwa walinyanyaswa wakiwa katika maandamano katika midani ya Tahrir.
'Tatizo liko kwa itikadi mbovu'
Watetesi hao wa haki wanasema kuwa polisi mara nyingi wanawalaumu waathiriwa kuliko wale wanaofanya uhalifu huo.
Sasa sheria hii inachukuliwa kama hatua kubwa sana kusaidia tatizo hilo, ila hofu ni kwa utekelezaji wake. Wadadisi wanasema kuwa itakuwa vigumu zaidi kubadilisha itikadi za watu juu ya unyanuasaji wa wanawake nchini humo .
Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz