AJALI MBAYA SANA YA BASI YAUAWA WATU ZAIDI YA AROBAINI :


0 comments:

TUNAOMBA RIDHI KWA PICHA HIZI: WABAKAJI SASA KATIKA MAUMIVU MAKALI BAADA YA KUVIMBA SEMU ZA SIRI:



kama unajua uwezi endelea kuangalia picha hizi ni bora ukaacha kabisa kama utaendelea bonyeza read more

0 comments:

BIBI BOMBA WAVURUGWA NA MAJANGA YA SNURA

 Msanii mkali wa kike tanzania anaetamba na wimbo wake wa NIMEVURUGWA Pia ni hil maker wa MAJANGA usiku wa jana alijikuta akitembelea maeneo ya excape 1 mikocheni kuonana na mabibi bomba baada ya kuomba kwa mda mrefu kukutana na mkali huyo alieimba wimbo wa majanga.,
 mabibi bomba wakiimba majanga na snura





 safffffi
 pozi kidogo lakuwavuruga wale wanaopenda swaga zako
 SNURA akipata msosi kabla yakuingia kwa bibi bombaz
 Babuu wa kitaa na SNURA
 SNURA na ISHA MASHAUZI
 T.i.D MZEE mnyama na snura
 Chidy beeenz na mamaa majanga



Mr manager hyperman hk akiingia na snura kwenye jumba la bata ndefu na bibi bomba

0 comments:

UPDATE:TAARIFA KAMILI KUHUSU BOMU KATIKA KANISA LA KKKT DAR ES SALAAM


POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.


Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana TMA.


"Baada ya kupata taarifa, polisi walifika eneo la tukio na kukuta kifaa kilicho katika umbo la kasha kikining'inia kwenye transfoma karibu na Kanisa kikiwa kinawaka taa.


“Katika kasha hilo kulikuwa na maandishi ya kalamu ya wino yaliyosomeka TMA na Airport," alisema Kamanda Kova.


Alisema baada ya uchunguzi wa awali, polisi walibaini kuwa kifaa hicho si bomu na kuondoka nacho kwa uchunguzi zaidi. Mtabiri Mwandimizi wa hali ya hewa kutoka TMA, Augustino Kanemba, alisema kifaa hicho kinaitwa Radio Sound na hutumiwa na Mamlaka hiyo kufanya utafiti wa hali ya anga za juu.


"Kifaa hiki hurushwa juu kuleta taarifa ya hali ya anga, kwa kawaida hufungwa puto ili kipae angani na baada ya kufika juu, puto hupasuka na kutua sehemu yoyote ya Dar es Salaam … hili si bomu," alisisitiza Kanemba.


Hata hivyo, Kamanda Kova alipongeza washarika wa Kanisa hilo, kwa kutoa taarifa Polisi na kuomba waendelee kufanya hivyo wanapoona kitu wasichokielewa.


Akizungumzia mlipuko katika Kanisa la KKKT, Usharika wa Segerea, Kamanda Kova alisema Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wataalamu wa fani za ugaidi na matumizi ya mabomu kutoka makao makuu ya Jeshi hilo, wanafanya upelelezi kubaini waliohusika na tukio hilo.


Katika tukio hilo la Agosti 24 mwaka huu saa 8 usiku, waumini wapatao 20 wakiwa wanaendelea na ibada, ghafla walitokea watu wanne na kuingia kanisani na kutupa chupa ya bia ikiwa na utambi na mafuta yadhaniwayo kuwa ya taa eneo la madhabau na kusababisha mlipuko.


Katika hatua nyingine, Polisi imekamata wahalifu 180 wakiwamo majambazi katika msako ulioendeshwa na Jeshi hilo ndani ya wiki moja. Pia imekamata bastola mbili, risasi tisa, magunia mawili ya bangi na magari mawili ya wizi.





0 comments:

UPDATE:TAARIFA KAMILI KUHUSU BOMU KATIKA KANISA LA KKKT DAR ES SALAAM


POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana TMA.
"Baada ya kupata taarifa, polisi walifika eneo la tukio na kukuta kifaa kilicho katika umbo la kasha kikining'inia kwenye transfoma karibu na Kanisa kikiwa kinawaka taa.
“Katika kasha hilo kulikuwa na maandishi ya kalamu ya wino yaliyosomeka TMA na Airport," alisema Kamanda Kova.
Alisema baada ya uchunguzi wa awali, polisi walibaini kuwa kifaa hicho si bomu na kuondoka nacho kwa uchunguzi zaidi. Mtabiri Mwandimizi wa hali ya hewa kutoka TMA, Augustino Kanemba, alisema kifaa hicho kinaitwa Radio Sound na hutumiwa na Mamlaka hiyo kufanya utafiti wa hali ya anga za juu.
"Kifaa hiki hurushwa juu kuleta taarifa ya hali ya anga, kwa kawaida hufungwa puto ili kipae angani na baada ya kufika juu, puto hupasuka na kutua sehemu yoyote ya Dar es Salaam … hili si bomu," alisisitiza Kanemba.
Hata hivyo, Kamanda Kova alipongeza washarika wa Kanisa hilo, kwa kutoa taarifa Polisi na kuomba waendelee kufanya hivyo wanapoona kitu wasichokielewa.
Akizungumzia mlipuko katika Kanisa la KKKT, Usharika wa Segerea, Kamanda Kova alisema Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wataalamu wa fani za ugaidi na matumizi ya mabomu kutoka makao makuu ya Jeshi hilo, wanafanya upelelezi kubaini waliohusika na tukio hilo.
Katika tukio hilo la Agosti 24 mwaka huu saa 8 usiku, waumini wapatao 20 wakiwa wanaendelea na ibada, ghafla walitokea watu wanne na kuingia kanisani na kutupa chupa ya bia ikiwa na utambi na mafuta yadhaniwayo kuwa ya taa eneo la madhabau na kusababisha mlipuko.
Katika hatua nyingine, Polisi imekamata wahalifu 180 wakiwamo majambazi katika msako ulioendeshwa na Jeshi hilo ndani ya wiki moja. Pia imekamata bastola mbili, risasi tisa, magunia mawili ya bangi na magari mawili ya wizi.



0 comments:

MWANAMKE ALIYEPANGA KUMUUA MUMEWE AENDELEA KUSOTA RUMANDE


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Arusha jana imekataa ombi la hati ya dharura ya dhamana ya mke wa mfanyabiashara maarufu wa madini mkoani Arusha, Janeth Jackson (32), anayedaiwa kupanga njama za kumuua mumewe wa ndoa.
Janeth na mshitakiwa wa pili, Novatus Elias kupitia Wakili wao, Samsoni Rumende waliwasilisha hati hiyo katika Mahakama Kuu, kuomba dhamana baada ya mahakama ya wilaya ya Arusha iliyoko Sekei, kuwanyima dhamana.
Mahakama iliwanyima dhamana washitakiwa hao, kwa maelezo kuwa kufanya hivyo ni kuharibu kesi, kwani kuna watuhumiwa wengine hawajakamatwa.
Hata hivyo, Jaji Mary Moshi alikataa kumjumuisha mshitakiwa wa pili katika hati hiyo, kwa maelezo kuwa wakili hakumjumuisha katika hati.
‘’Katika hati ya dharura, naona jina la mshitakiwa wa kwanza tu ndiye anayeombewa dhamana, lakini jina la mshitakiwa wa pili, Elias, haliko hivyo siwezi kusikiliza kwa kuwa ni kinyume na utaratibu,’’ alisema Jaji Moshi.
Pamoja na hayo, Jaji Moshi alimnyima dhamana Janeth kwa maelezo kuwa Wakili Rumende amefanya makosa ya kisheria, kwani alipaswa kukata rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama ya wilaya wa kumnyima dhamana mteja wake.
Alisema kuomba hati ya dharura ya kuomba dhamana, sio utaratibu wa kisheria na kutokana na hali hiyo, alimtaka wakili huyo kwenda kujipanga upya .
Awali akizungumza mahakamani hapo, Rumende alimwomba Jaji Moshi kumpa dhamana mteja wake, kwani ana mtoto mchanga wa miezi mitano.
Rumende alidai kuwa dhamana ni haki ya msingi ya mteja wake na hawezi kuathiri mwenendo wa kesi na atatii masharti ya dhamana kwa jamii, inayomzunguka bila ya wasiwasi wowote.
Hoja hizo zilipingwa vikali na Wakili wa Serikali, Edana Kasala aliyedai kuwa utaratibu umekiukwa na pili mahakama ya wilaya iko sahihi kuwanyima dhamana washitakiwa hao.
Janeth ambaye ni mkazi wa Moshono, jijini Arusha pamoja na Novatus Elias, katika kesi hiyo katika mahakama ya wilaya, wanashitakiwa kwa kula njama ya kutaka kumwua Jackson Manjuru ambaye ni mume wa Janeth.
Washitakiwa wote wawili pia wanadaiwa kutenda kosa la kula njama na kutaka kumwua Desderi Sabas, anayeishi Bukoba mkoani Kagera, ambaye ni mtoto wa nje wa mume huyo.
Washitakiwa wote hawakutakiwa kujibu lolote mahakamani hapo, kwa sababu Mahakama hiyo kisheria haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.


Read more: http://talkbongo.blogspot.com/2013/08/mwanamke-aliyepanga-kumuua-mumewe.html#ixzz2d9sJk2Ke

0 comments:

DEMU MKENYA,AFUNGUKA UHUSIANO WAKE NA DIAMOND


Demu Mkenya Angel Maggy, aliyedaiwa kutoka na Staa wa Bongo Fleva Nasib Abdul‘Diamond Platinum’ambaye ni mtangazaji wa kipindi cha Tujuane cha kituo cha Tv cha KTN cha nchini humo amefunguka na TEENTZ kuhusiana na uhusiano wake na msanii huyo wa Bongo


Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Jijini Nairobi alisema kuwa hana uhusiano na msanii huyo na anashangaa hayo maneno kusambaa na kwamba yeye ni shabiki mkubwa wa Diamond.
‘No …Diamond is apal lyk any other..yy shld I date him??Am not in love with him’alisema Angel.
Alipoulizwa kwanini ameamua kuchora tattoo ya msanii huyo kwenye mkono wake alisema kuwa kuchora…


Jast tat I got atattoo named diamond doesn’nt mean ama dating him’alisema Angel.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari za burudani vya Kenya, zilisema kuwa ishu ya kutoka na Diamond ilianza kuvuma mara baada ya kufanya shoo mbili katika Miji ya Nairobi na Mombasa nchini humo,ambapo aliporejea Bongo ndipo ukaibuka mlipuko wa habari zilizomhusu na mrembo huyo.


Jast tat I got atattoo named diamond doesn’nt mean ama dating him’alisema Angel.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari za burudani vya Kenya, zilisema kuwa ishu ya kutoka na Diamond ilianza kuvuma mara baada ya kufanya shoo mbili katika Miji ya Nairobi na Mombasa nchini humo,ambapo aliporejea Bongo ndipo ukaibuka mlipuko wa habari zilizomhusu na mrembo huyo.

Ilisemekana kuwa alipokuwa akifanya shoo kwenye Ukumbi wa KICC, Nairobi siku ya kwanza, Diamond aliimba wimbo wake wa Ukimuona maalum (dedication) kwa ajili ya Angel, jambo lililomfanya mrembo huyo kuonekana ‘spesho’ miongoni mwa maelfu waliohudhuria onesho hilo.

Imeripotiwa kuwa baada ya shoo hiyo kumalizika USIKU, Angel alionekana ‘beneti’ na Diamond wakielekea katika hoteli aliyofikia staa huyo Nairobi.

0 comments:

MAJANGA:BIASHARA YA NGONO YARUHUSIWA RASMI KUFANYIKA KWENYE MAGARI BARABARAN



“Jiji limehalalisha na kufungua vyumba 9 ambavyo vitatumiwa na machangudoa na wateja wao kihalali na kwa usalama zaidi” 
Drive-in ya ngono imefunguliwa rasmi, Zurich katika mkakati wa kuwalinda makahaba ili kuhamisha biashara ya umalaya nje ya mji wa Swiss.


Vibanda(pichani kulia) tisa vya ngono vilivyojificha ndani ya uzio mkubwa vimeandaliwa kwaajili ya wauza miili ‘malaya’ na wateja wao kuanzia leo na kuendelea.

Kuna saini ndogo inayoonesha muda wa kazi, mwamvuli mwekundu kutambulisha eneo hilo kama eneo la shughuli hiyo ambalo zamani lilikuwa ni eneo la viwanda magharibi mwa jiji hilo. 

Pamoja na hayo kuna sharia maalumu zimewekwa(kushoto pichani). Mteja lazima awe na umri usiopungua miaka 18, mtu mmoja tu kwenye gari, na kondom lazma itupwe kwenye vyombo maalumu baada ya kutumika.

Kuna eneo ambalo mteja anaweza kuchagua mwanamke anayemfaa, pamoja na makubaliano ya bei kabla ya kuelekea kwenye kibanda, ambacho ni cha mbao kinacho fanana na eneo la kuegesha gari.

Kila kiboksi kina alamu ili kuwalinda Malaya hao.

Michael Herzig, mkurugenzi katika huduma ya jamii ya wafanyakazi wa ngono jijini alisema “Umalaya ni biashara” 

“Hatuwezi kuzuia, hivyo tunataka kudhibiti ili kuwasaidia wafanyakazi wa ngono na jamii, sababu bila kufanya hivyo uhalifu unaongezeka na wahuni wanazidi kuwa wengi” 



Ursula Kocher, Mkurugenzi wa Flora Dora, mtandao unaounga mkono Malaya, alisema kuwa machangu doa mara nyingi huchukuliwa na kupelekwa porini au nje ya mji na kujikuta katika mazingira hatari.

Alisema “ hapa wanabakia humuhumu ndani na kuhudumia wateja wao haraka” 

Eneo hilo la drive-in ya ngono limehalalishwa na wakazi wa Zurich katika sharia ya mwezi machi, 2012baada ya kupigiwa kura kwa asilimia 52.6 kukubaliana nalo.

Eneo hilo pia lina makubaliano mazuri tu yanayohusisha vyama vyote vya siasa nchini humo, likiwa na wanachama wengi wa chama cha Swiss People's Party (SVP) wanaopinga mpango huo.

"haitofanikiwa, labda kwasababu wateja hawatokuja au eneo hilo halitotumiwa na machangudoa” alisema Sven Oliver Dogwiler, mwanasiasa wa eneo hilo ambae ni mwanachama wa SVP

0 comments:

WAKENYA WAWILI WAKUBALIANA KUMUOA MWANAMKE MMOJA...



Mwendwa ni mmoja wa wanaume hao walioamua kugawana mke mmoja.


Wanaume wawili nchini Kenya wameibuka na mbinu isiyo ya kawaida ya kupata suluhu ya kupigania mwanamke ambaye wote wanampenda Wamesaini mkataba wakikubaliana kuishi nae kwa zamu.
Silvester Mwendwa ni mmoja wa wanaume hao. Ameeleza BBC kwanini binafsi anamuhusudu mwanamke huyo.
Mmoja ya wa wanaume hao alisema haoni ubaya wowote kwa yeye na mwenzake kumuoa mwanamke mmoja.
Amehoji sheria ya sasa inayoruhusu wanaume kuoa wanawake wengi na wakati huo huo kuharamisha mpango kama huo kwa kina mama.
Sylvester Mwendwa anasema wazazi wake wamekubali na mpango wake na wako tayari kumtolea mahari.
Wanaume hao wawili walikubali kumuoa mwanamke huyo baada ya kugundua kwamba kumbe wote wana uhusiano wa kimapenzi naye.
Na kumbe mwanamke huyo alikuwa ameahidiana na kila mmoja wao kwamba angefunga nao ndoa bila ya wao kujuana.
Lakini walipogunduana , ilikuwa ni ugomvi kwa mara kwa mara lakini mwanamke huyo alipoambiwa amchague mnmoja wao, alishindwa. Akasema anawapenda wote wawili.
Na baada ya hapo watatu hao waliafikiana kusaini mkataba ambao utaruhusu wanaume hao wawili kuishi na mwanamke huyo kama bwana na bibi ila kila mmoja wao atakuwa na wakati wake wa 'kwenda kumjulia hali.'
Vile vile mkataba huo unawashurutisha kugawana majukumu yote ya nyumbani ikiwa ni pamoja na kuwalea watoto na kutowabagua kwa kuwa wote watakuwa na haki sawa.
Hata hivyo kwa mujibu wa sheria za kenya ni haramu kwa mwanamke kuolewa na wanaume wawili na mkataba huo sasa umeibua mjadala mkali wa kisheria, huku sheria mpya ya ndoa ikitarajiwa kujadiliwa na kuidhinishwa bungeni.


Read more: http://talkbongo.blogspot.com/2013/08/wakenya-wawili-wakubaliana-kumuoa.html#ixzz2d9p9OQTC

0 comments:

Magazeti ya leo August 27 2013 Udaku, Michezo na Hardnews



.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz