SOMA HAPA WABUNGE WA CCM JUZI WALIVYORUSHIANA MANENO MAZITO KUHUSIANA NA KUUZWA KWA UDA



MBUNGE wa Urambo Magharibi, Prof. Juma Kapuya (CCM), ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi wa zamani, jana alijikuta katika wakati mgumu wa kuumbuliwa na mbunge mwenzake wa Temeke, Abbas Mtemvu (CCM), wakati wawili hao wakibishania uuzwaji tata wa Kampuni ya Usafiri Dar es Salaam (UDA).Hatua hiyo ilijitokeza wakati Mtemvu akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa mwaka wa fedha 2014/2015, na kuungana na wabunge wenzake kadhaa waliotangulia kuchangia, akidai UDA imeuzwa kifisadi bila wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam kushirikishwa.
 Wakati Mtemvu akiendelea kujenga hoja yake, Prof. Kapuya aliomba kumpa taarifa, akimweleza kuwa mbunge kujishughulisha na uwekezaji si dhambi na kwamba UDA imeuzwa kihalali wala hakuna ufisadi kama inavyodaiwa, isipokuwa mbunge huyo anatumika kuwashawishi wabunge kupinga suala hilo. Baada ya Prof. Kapuya kuketi,

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz