Wandishi wa BBC washambuliwa Urusi


BBC imeitaka serikali ya Urusi kuchunguza tukio hilo dhidi ya wandishi wake

BBC imewasilisha malalamiko kwa serikali ya Urusi baada ya wandishi wake wa habari kushambuliwa Kusini mwa nchi hiyo.

Wandishi hao walikuwa nchini Urusi kuchunguza madai ya baadhi ya maafisa wa usalama wa Urusi kuuawa karibu na mpaka na Ukraine.

Baada ya kuwaarifu maafisa wa huduma ya dharura , waandishi hao walipelekwa katika kituo cha polisi na kuhojiwa kwa saa nne.

Picha walizokuwa wamenasa kwenye kamera zilifutwa wakati wakiwa kwenye kituo cha polisi.

BBC inasema kuwa imechukizwa na kitendo hicho na kutoa wito kwa maafisa wa utawala nchini humo kuchunguza taarifa hizo pamoja na kuwataka kulaani kitendo hicho.

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz