SEREKALI KUPAMBANA NA WACHAFUZI WA MAZINGIRA JIJINI ARUSHA







Wakazi waishio katika kata ya olasiti jijini arusha wameipongeza manispaa ya jiji hilo  kwa kufanikiwa kwa kiasi kikubwa  kudhibiti utupaji wa taka ovyo  katika maeneo ya makazi wanapo ishi

Hayo yamesemwa na mmoja  wa wakazi hao akifaamika kwa majina ya Jacob marugas alipozungumza na waandishi wa habari kujua mafanikio yaliofikiwa na manispaa ya jiji hilo katika swala la usafi wa mazingira na kujionea mabadiliko makubwa tofauti nahapo awali

Pia ameongeza kuwa swla la magari kupita kila ijumaa saa nne ni tatizo hivyo ombi ni kuongezwa kwa magari nay awe ni yakupita angalau mara tatu katika wiki  ili kuepusha tatizo la uchafu kukaa kwa mda mrefu

Hata hivyo wito wake kwa serekali ni manispaa  ya jiji la arusha kuongeza idadi ya magari  ya kubebea taka  pamoja na vitendea kazi kwa wafanya kazi  pia ameitaka manispaa hiyo kupanga utaratibu mzuri wa kuwa ni sehemu gani maalumu ya wakzi kukusanya taka ili kuepuka usumbufu wa magari kushindwa kuingia

0 comments:

Copyright © 2012 KARINGA NEWS Tz